logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Video) "Kifo umepeleka Kibaki wapi?" Embarambamba amwomboleza Kibaki katika wimbo

Embarambamba anaoneka akisakata densi katika shamba la mahindi, akipanda miti na kujibingirisha matopeni

image
na Radio Jambo

Habari27 April 2022 - 05:20

Muhtasari


•Video ya wimbo huo inaonyesha Embarambamba akisakata densi katika shamba la mahindi, akipanda miti na kujibingirisha matopeni.

Mwanamuziki mashuhuri Christopher Nyangwara Mosioma almaarufu Embarambamba ametoa kibao kipya maalum kwa Hayati Mwai Kibaki.

Embarambamba ambaye anatambulika sana kutokana na mtindo wake tatanishi wa kucheza densi unaohusisha sarakasi nyingi amemwomboleza rais huyo wa zamani katika wimbo huo 'Kibaki'.

Katika wimbo huo, Embarambamba amebainisha kuwa  Wakenya watampeza sana rais huyo wa zamani hasa kutokana na hotuba zake zenye ucheshi.

"Kibaki eeh Kibaki. Kibaki amekufa Kibaki (*2) Kifo, Kifo umechukua Kibaki wapi?" Sehemu ya wimbo wa Embarambamba inasema. 

Msanii huyo kutoka Kisii alimtambua Hayati kwa kuzindua elimu bila malipo, kukuza uchumi na kukubali kugawana serikali na Raila Odinga.

Video ya wimbo huo inaonyesha Embarambamba akisakata densi katika shamba la mahindi, akipanda miti na kujibingirisha matopeni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved