logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bahati kuwania kiti cha ubunge wa Mathare kwa tikiti ya Jubilee

Kioni alisema chama hicho kilikuwa na masilahi ya vijana moyoni na hivyo kuamua kurejesha cheti cha Bahati.

image
na Radio Jambo

Habari13 May 2022 - 11:23

Muhtasari


  • Kioni alisema chama hicho kilikuwa na masilahi ya vijana moyoni na hivyo kuamua kurejesha cheti cha Bahati

Mwanamuziki Kevin Kioko almaarufu Bahati sasa atawania kiti cha ubunge cha Mathare baada ya Chama cha Jubilee kufanya mabadiliko katika uamuzi wake wa kuondoa cheti chake cha uteuzi.

Tangazo hilo lilitolewa na Katibu Mkuu wa Jubilee, Jeremiah Kioni, wakati wa kikao na wanahabari katika makao makuu ya chama hicho jijini Nairobi.

Kioni alisema chama hicho kilikuwa na masilahi ya vijana moyoni na hivyo kuamua kurejesha cheti cha Bahati.

Kiti cha ubunge cha Mathare kilitengwa kwa ajili ya chama cha ODM.

Uamuzi huo ulizua ghadhabu miongoni mwa wagombea ambao walikuwa wakitazama viti mbalimbali vya kuchaguliwa lakini walifungiwa nje kwa sababu ya kupangiwa maeneo.

Haya yanajiri wiki chache baada ya msanii huyo kukejeliwa sana mitandaoni baada ya kulia akiwahotubia wanahabari, sababu ya kunyang'anywa cheti cha chama hicho.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved