logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kurt Zouma: Beki wa West Ham akiri kosa la kumpiga paka wake

Yoan, 24, alirekodi tukio hilo, ambalo lilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

image
na Radio Jambo

Makala24 May 2022 - 13:30

Muhtasari


  • Kaka yake Zouma Yoan, anayechezea Dagenham na Redbridge, alikiri kosa moja baada ya uchunguzi wa RSPCA

Beki wa West Ham United Kurt Zouma amekiri kosa la kumpiga teke na kumpiga paka wake kwenye video ambayo pia ilimuonesha akisema "Naapa nitamuua".

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alikiri makosa mawili chini ya Sheria ya Ustawi wa Wanyama katika katika Mahakama ya Thames.

Kaka yake Zouma Yoan, anayechezea Dagenham na Redbridge, alikiri kosa moja baada ya uchunguzi wa RSPCA. Yoan, 24, alirekodi tukio hilo, ambalo lilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

Kesi imeahirishwa hadi Juni 1. Anwani za ndugu hao zilizuiwa kufuatia agizo la mahakama.

Mahakama ilielezwa kuhusu picha za video za kutatanisha za tukio hilo, ambazo zilinakiliwa nyumbani kwa mchezaji huyo wa West Ham na kuchapishwa kwenye Snapchat na emoji za 'kucheka' na kaka yake tarehe 6 Februari.

Zouma alionekana akimzungusha paka huyo, kabla ya kumrushia jozi ya viatu na kumpiga kichwani.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved