logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ulikuwa maskini,'Amberay amfokea ex wake

Utengano wake wa hivi majuzi na mwanamume wake hata hivyo, umekuwa wa kipekee

image
na Radio Jambo

Habari11 June 2022 - 20:49

Muhtasari


  • Utengano wake wa hivi majuzi na mwanamume wake hata hivyo, umekuwa wa kipekee kwa kuwa wamekuwa wakirushiana vijembe kwenye mitandao

Mwanasosholaiti wa Kenya Faith Makau, anayejulikana pia kama Amberay, amezua taharuki mpya mtandaoni baada ya kumvamia mpenzi wake wa zamani na kusema haya kumhusu.

Amberay ni mmoja wa watu mashuhuri wa Instagram nchini Kenya, mama wa mtoto mmoja, anayejulikana sana kwa tabia yake ya kuwa kwenye uhusiano mmoja hadi mwingine.

Sio mtu mashuhuri wa Kenya pekee anayefanya hivi; wengine wachache hufanya vile vile. Amberay amekuwa akichumbiana, kuachwa, na kuhama huku wote wawili wakiendelea na maisha yao.

Utengano wake wa hivi majuzi na mwanamume wake hata hivyo, umekuwa wa kipekee kwa kuwa wamekuwa wakirushiana vijembe kwenye mitandao ya kijamii bila kurudi nyuma.

Amberay aliingia kwenye Instagram na kuchapisha ujumbe ambao kila mtu anaamini ulikusudiwa kwa mpenzi wake wa zamani, akidai kuwa aliachana naye kwa sababu alikuwa maskini.

"Sijui ni nani anayehitaji kusikia haya lakini…Mwanamke ambaye hakukuoa kwa sababu ulikuwa maskini au si wa aina yake, kuna uwezekano mkubwa atapata mwanamume mzuri anayelingana na vigezo vyake na kuishi kwa furaha siku zote. Hapana, hatateseka au kujuta. Acha kutazama filamu nyingi za Sierra Leone.🤭,"Amber Aliandika.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved