logo

NOW ON AIR

Listen in Live

TSC yakana madai ya kuzuia walimu kuhudumu kama maafisa wa IEBC uchaguzini

Madai yaliibuka yakiashiria kuwa walimu hawataruhusiwa kuchukua kazi za IEBC.

image
na Radio Jambo

Habari23 June 2022 - 04:59

Muhtasari


• Ripoti hiyo pia ilionyesha kuwa TSC imewaagiza wakuu wa shule kutowapa walimu ruhusa kuchukua kazi hizo.

• Nafasi zilizotangazwa zilijumuisha maafisa Wasimamizi, Naibu Maafisa Wasimamizi na kazi za ukarani miongoni mwa zingine.

Ripoti kuwa Tume ya Kuajiri Walimu nchini TSC imepiga marufuku walimu kuchukua kazi za muda za IEBC ni feki.

Madai yaliibuka yakiashiria kuwa walimu hawataruhusiwa kuchukua kazi za IEBC.

Ripoti hiyo pia ilionyesha kuwa TSC imewaagiza wakuu wa shule kutowapa walimu ruhusa kuchukua kazi hizo.

TSC hata hivyo, amekanusha ripoti hizo na kusema kwamba habari hizo ni za uongo na za kupotosha.

Katika tweet iliyo na picha ya skrini ya ripoti hiyo ghushi, TSC ilisema: " Tume imevutiwa na habari hizi za uongo. Zichukulieni kwa dharau inayostahili".

Ripoti hiyo ya kupotosha ilijiri wakati ambapo IEBC inawaorodhesha watu waliotoa maombi kwa kazi mbalimbali za muda ilizotangaza wiki zilizopita kwa sababu ya kuendesha uchaguzi mkuu wa Agosti 9, mwaka huu.

Nafasi zilizotangazwa zilijumuisha maafisa Wasimamizi, Naibu Maafisa Wasimamizi na kazi za ukarani miongoni mwa zingine.

Duru za kuaminika zimesema kwamba walimu wengi kote nchini ni miongoni mwa waliowekwa kwenye orodha fupi ya mchujo.

Wale walioitwa kwenye mchujo wanashauriwa kuhudhuria kwani hakuna amri ya kuwazuia kuchukua kazi ikiwa watafaulu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved