logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu wanne wafariki dunia na wengine 132 kujeruhiwa kwenye ajali ya treni Tanzania

Jeshi la Polisi wameeleza kuwa wanaendelea na uchunguzi wa chanzo cha ajili hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari23 June 2022 - 04:28

Muhtasari


• Taarifa kutoka TRC zinasema kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 5 za asubuhi leo ambapo mabehewa nane yaliyokuwa na jumla ya abiria 930 yalianguka katika eneo la Malolo.

Watu wanne wamefariki dunia na wengine 132 kujeruhiwa kwenye ajali ya treni iliyotokea Tabora, Magharibi mwa Tanzania, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limethibitisha.

Taarifa kutoka TRC zinasema kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 5 za asubuhi leo ambapo mabehewa nane yaliyokuwa na jumla ya abiria 930 yalianguka katika eneo la Malolo.

Katika taarifa hiyo, ilieleza kuwa majeruhi wamefikishwa katika hospitali ya Mkoa ya Kitete kwaaajili ya matibabu huku manusura wakitafutiwa utaratibu wa kumalizia safari zao.

Hata hivyo waliodhibitika ni watoto wawili, mmoja wa kiume na mmoja wa kike. Sambamba na hao wamefariki watu wazima wawili mmoja akiwa ni mwanamke.

Jeshi la Polisi wameeleza kuwa wanaendelea na uchunguzi wa chanzo cha ajili hiyo.

Matukio ya ajali za treni yametokea mara kadhaa ambapo mwanzoni mwa mwaka huu, treni iliyokuwa ikisafiri Arusha kwenda Dar es Salaam ilipata ajali katika eneo la Pangani, Tanga na kusababisha kifo cha mmoja na majeruhi watano.

Mwaka jana, ajali nyingine ilitokea Bahi- Dodoma ambapo watu watatu walipoteza maisha na wengine 66 kujeruhiwa.

Ikumbukwe mwaka 2002, abiria 280 walipoteza maisha kwenye ajali iliyokea Dodoma.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved