logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cristiano Ronaldo aomba kuondoka Manchester United

Ronaldo aligombana na Harry Maguire katika nafasi ya unahodha wa United msimu uliopita.

image
na Radio Jambo

Habari03 July 2022 - 04:16

Muhtasari


•Ronaldo anataka Manchester United kumwachilia aondoke katika klabu hiyo iwapo watapata ofa bora.

•Ronaldo aligombana na Harry Maguire katika nafasi ya unahodha wa United msimu uliopita.

Manchester United imebanduliwa kutoka Champions League

Cristiano Ronaldo anataka Manchester United kumwachilia aondoke katika klabu hiyo iwapo watapata ofa bora kwa ajili yake msimu huu wa joto.

Mshambuliaji huyo wa Ureno, 37, alirejea Old Trafford kutoka Juventus msimu uliopita wa joto.

Hata hivyo, licha ya kuwa mfungaji bora wa United msimu uliopita - na wa tatu katika Premier League - kampeni yote kwa jumla ilionekana kuwa ya kukata tamaa .

United walimaliza katika nafasi ya sita kwenye ligi ya Premier  hivyo wakakosa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.

Hiyo ina maana kwamba Ronaldo, ambaye amesalia na mwaka mmoja kwenye mkataba wake na United pamoja na mwaka wa hiari, atacheza katika Ligi ya Europa kwa mara ya kwanza.

Sio kitu anachofurahia na mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d'Or anahisi kunaweza kuwa na chaguo la kuvutia zaidi katika kipindi hiki katika maisha yake ya soka.

Mchezaji huyo atasalia Mancheter United licha ya kuhusishwa na uhamisho wa kujiunga na Chelsea.

Fowadi huyo wa zamani wa Real Madrid ana wasiwasi akisisitiza kuwa anaiheshimu United lakini anapoingia katika hatua za mwisho za maisha yake ya soka, anataka kuwania tuzo kubwa zaidi.

United bado haijasema lolote kuhusu mustakabali wa Ronaldo, ingawa awali vyanzo vya habari viliamini kwamba Mreno huyo angesalia Old Trafford msimu ujao.

Ingawa itakuwa pigo kwa United ikiwa wangempoteza mmoja wa wachezaji bora zaidi ambao wamewahi kuwa nao, pia ingesuluhisha maswala machache kwa meneja mpya Erik ten Hag.

Ronaldo aligombana na Harry Maguire katika nafasi ya unahodha wa United msimu uliopita, huku hamu ya kocha wa muda Ralf Rangnick ya kutekeleza mtinfo wake ikizimwa na Ronaldo aliyekataa kushiriki katika mfumo kama huo.

Ingawa Ten Hag amesema ni kwa kiasi gani anatazamia kuungana na Ronaldo, haijabainika ni kwa namna gani uchezaji wa fowadi huyo utaendana na Mholanzi huyo.

Zaidi ya hayo, Ronaldo ndiye mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi kwenye Ligi Kuu ya England na kuondoka kwake kungeleta wigo zaidi ndani ya bajeti ya United ya msimu wa joto.

Ronaldo anatarajiwa kurejea klabuni hapo kwa mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wiki hii. Inatarajiwa atakuwa kwenye ziara yao ya maandalizi ya msimu mpya nchini Thailand na Australia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved