logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafcon: Michuano ya Kombe la Afrika miongoni mwa wanawake yarudi

Itaandaliwa katika ardhi ya Afrika Kaskazini kwa mara ya kwanza na Morocco.

image
na Radio Jambo

Habari03 July 2022 - 10:25
Wachezaji wa Nigeria

Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika miongoni mwa Wanawake (WAFCON) inarejea mwezi huu baada ya kukosekana kwa miaka minne, huku mashindano makubwa zaidi ya wanawake barani humo yakipanuka na kushirikisha timu 12.

Baada ya kuonyesha vipaji vya hali ya juu kutoka kwa Mnigeria Mercy Akide-Udoh katika miaka ya 1990 hadi fowadi wa Afrika Kusini Thembi Kgatlana mara ya mwisho, mashindano ya mwaka huu pia yataamua mechi nne za Afrika za kufuzu kwa Kombe la Dunia la Wanawake 2023.

Itaandaliwa katika ardhi ya Afrika Kaskazini kwa mara ya kwanza na Morocco, huku michezo ikichezwa katika viwanja vitatu vya Rabat na Casablanca kuanzia Julai 2-23.

Nigeria ilinyanyua kombe hilo katika matoleo matatu yaliyopita na wameshinda mara tisa katika WAFCON 11 zilizopita, na timu hiyo iliyoorodheshwa juu zaidi barani bado ndiyo timu itakayotoa ushindani mkali katika kinyang’anyiro hicho

Cameroon na Afrika Kusini ni miongoni mwa wapinzani wao wa karibu, lakini kutokana na nchi nne kushiriki kwa mara ya kwanza huenda mambo yasiwe rahisi


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved