logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto: Uhuru alikataa Maaskofu wasitupatanishe, nimemvumilia sana, amekuwa akinidhalilisha

Ruto - "Kule kudhalilishwa ambako nimeoneshwa kutoka kwa bosi wangu, hakuna mtu mwingine angeweza kustahimili,”

image
na Radio Jambo

Habari08 July 2022 - 06:40

Muhtasari


• "Uliza maaskofu, uliza Askofu wa ACK, Uhuru alikataa tusipatanishwe” - Ruto

Naibu rais na kiongozi wa Kenya Kwanza

Hatimaye, naibu wa rais William Ruto amezungumzia kilichotokea baina yake na bosi wake rais Uhuru Kenyatta mpaka kupelekea urafiki wao uliokuwa umeshuhudiwa bayana tangu mwaka 2013 kuzorota na wawili hao kuanza kutupiana mabomu mazito ya maneno.

Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na kituo kimoja cha runinga humu nchini katika ukumbi wa mgahawa wa Serena jijini Nairobi, Ruto alielezea kwamba rais Uhuru Kenyatta ndiye mwenye kulaumiwa kwa kuzorota kwa urafiki wao kwani hata maaskofu walijaribu kuwapatanisha lakini Kenyatta akakataa na kuchagiza zaidi uhasama wao.

“Kwa kweli ni kwa bahati mbaya sana na ninajuta pakubwa kwa sababu ni moja kati ya vitu ambavyo sikuwa navitegemea kabisa kukosana na bosi wangu. Acha niseme ukweli, nimekuwa mtu mwenye Subira sana. Kule kudhalilishwa ambako nimeoneshwa kutoka kwa bosi wangu, hakuna mtu mwingine angeweza kustahimili,” alisema Ruto.

Kinara huyo wa muungano wa Kenya Kwanza pia alisema kwamba dharau ambazo Uhuru Kenyatta amemuonesha wangekuwa ni wengine kama Raila au Martha Karua, mambo yangekuwa mabaya sana ila kwa sababu yeye ni mwenye Subira, amejitahidi sana muda mrefu kutojibizana na mkubwa wake, Uhuru Kenyatta.

Aidha, Ruto alipuuzilia mbali madai yanayosemekana kwamab amewahi mdhalilisha Uhuru na kusema kwamab yeye mwenyewe alikuwa na mazungumzo na Kenyatta ambapo alimtaka atoe Ushahidi wa video inayoonyesha kwamba amemdhalilisha lakini rais Kenyatta akakana kwamba hakuna kitu kama hicho.

“Maaskofu walizungumza na mimi, wakaenda wakazungumza na rais Kenyatta na waliporejea kwangu niliwaambia nataka watupatanishe na Kenyatta, lakini yeye alikataa. Uliza maaskofu, uliza Askofu wa ACK,” Ruto alitema ukweli.

Akizungumzia madai ya kutaka kumzaba kofi rais, Ruto alisema kwamba ile ilikuwa lugha ya kimafumbo tu na ambayo sasa wapinzani wake wa kisiasa wanaitumia nje ya muktadha halisi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved