logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila amkashifu Ruto kwa kumlaumu kuhusu kupanda kwa bei ya unga

Mnamo 2017, Raila alitishia kuwafichua waliohusika na uagizaji wa mahindi kutoka nje

image
na Radio Jambo

Habari08 July 2022 - 20:53

Muhtasari


  • Raila alimtupia lawama Naibu Rais akisema aliwezesha uagizaji wa mahindi na kusababisha bei ya juu ya unga nchini

Mgombea urais wa Azimio Raila Odinga sasa anasema ni upuuzi kwa mpinzani wake wa Kenya Kwanza William Ruto kumlaumu kwa kupanda kwa bei ya unga.

Raila alimtupia lawama Naibu Rais akisema aliwezesha uagizaji wa mahindi na kusababisha bei ya juu ya unga nchini.

"Unajua wamekuwa wakilalamika kuwa gharama ya maisha ni kubwa...Waulize walioleta mahindi kutoka Mexico. Yeye (Ruto) ndiye aliyeharibu soko la mahindi hapa," Raila alisema.

Raila alizungumza Ijumaa wakati wa mkutano wa kampeni huko Lugari, kaunti ya Kakamega.

Mnamo 2017 na 2020, serikali iliruhusu uingizaji wa mahindi kutoka Mexico ili kupunguza upungufu huku wakulima wakisubiri msimu wa mavuno.

Ruto amekuwa akimsuta kiongozi huyo wa ODM akidai handshake kati yake  na Rais Uhuru Kenyatta 2018 ndio sababu ya bei ya unga kupanda.

“Mnamo 2018, pakiti ya kilo 2 ya unga wa mahindi iligharimu Sh75. Sasa inauzwa kwa Sh250 na tunaambiwa kwamba baada ya kupigwa kiwiko, [ni] yule jamaa wa Azimio,” alisema wakati wa mkutano huko Kilifi mnamo Juni 26.

Ruto alidai Raila alikuwa akimpa Uhuru ushauri mbaya, na kusababisha gharama ya juu ya maisha kwa sasa.

Mnamo 2017, Raila alitishia kuwafichua waliohusika na uagizaji wa mahindi kutoka nje, na kudai DP ni miongoni mwa waliohusika.

Alisema utaratibu wa kuagiza mahindi kutoka nje ya nchi ulikuwa wa samaki na anashangaa imekuwaje kwa muda mfupi usafirishaji huo kufika nchini Kenya.

Matamshi yake Raila yanairi siku moja tu bada ya wakenya kutishia kususia kupiga kura mnamo Agosti iwapo bei ya bidhaa muhimu haitapunguzwa.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved