logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alikiba: Siwezi enda kumuona R Kelly jela hata nikapewa nafasi, vitendo vyake sivisapoti!

“Labda ni vizuri kutuma salamu kuliko kuenda kuonana naye,” Alikiba alisema.

image
na Radio Jambo

Habari12 July 2022 - 12:56

Muhtasari


• "Vitu alivyovifanya mimi siwezi kuviunga mkono. Mimi binafsi nitaona aibu,” - Alikiba

Wasanii R Kelly na Alikiba

Msanii mkongwe katika gemu la bongo fleva, Alikiba ameweka wazi hisia zake kuhusu hukumu ya msanii kutoka Marekani, R Kelly ambaye alifungwa wiki chache zilizopoita kutokana na kesi ya muda mrefu iliyokuwa inamhusisha na unyanyasaji wa kingono.

Akizungumza katika mahojiano ya kituo kimoja cha redio nchini Tanzania, Alikiba alisema kwamba akipata nafasi ya kumtembelea R Kelly gerezani, atakubali kuenda lakini hajui kabisa atamwambia nini nguli huyo wa zamani wa muziki kwa sababu vitendo alivyohukumiwa navyo ni vya aibu na wala yeye haviuingi mkono kabisa.

“Nikipata nafasi ya kumtembelea R Kelly gerezani nitaenda lakini sijui nitaongea naye nini, vitu alivyovifanya mimi siwezi kuviunga mkono. Mimi binafsi nitaona aibu,” alisema mkurugenzi huyo wa Kings Music rekodi lebo.

Vile vile Alikiba alizidi kuelezea kwa kusema kwamba kama kutatokea majibu mawili ya kuchagua kati ya kumtembelea R Kelly gerezani na kutuma salamu tu basi atalichagua la pili na kughairi kuenda kuonana naye uso kwa uso.

“Labda ni vizuri kutuma salamu kuliko kuenda kuonana naye,” Alikiba alisema.

Ikumbukwe Alikiba aliwahi shirikishwa katika kibao kimoja na msanii huyo miongoni mwa mastaa wengine kama vile Navio, Amani, 2face Idibia, Fally Ipupa miongoni mwa majina mengine makubwa kutoka bara la Afrika kwa kibao kali kilichovuma kwa jina ‘Hands Across The World’

Msanii R Kelly alihukumiwa wiki juzi baada ya kupatikana na hatia ya kutumia ustaa wake kuwanyanyasa wanawake na watoto kingono pamoja na kuonesha picha za utupu wao.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved