logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Habari za hivi sasa! Mahakama ya juu yamtoa Sonko kinyang'nyironi

Majaji saba wakiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome walitaja kutokuwa na mamlaka kushughulikia rufaa hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari15 July 2022 - 13:21

Muhtasari


• Habari za hivi sasa! Mahakama ya juu yamtoa Sonko kinyang'nyironi 

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko

Habari za hivi sasa! Mahakama ya juu yamtoa Sonko kinyang'nyironi 

Safari ya Sonko kutafuta  ugavana wa Mombasa huenda imetiwa kikomo baada ya mahakama ya Juu siku ya Ijumaa kutupilia mbali rufaa yake.

Mahakama hiyo ilishikilia maamuzi ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa, ikithibitisha kuondolewa kwa aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko.

Katika uamuzi huo, mahakama kuu ilikubaliana na maamuzi ya mahakama ya chini ya kuunga mkono kuondolewa kwake afisini na Seneti.

Majaji saba wakiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome walisema walitupilia mbali rufaa ya Sonko kwa kukosa mamlaka ya kushughulikia swala hilo.

Mahakama ya Juu ilisikiliza rufaa hiyo ambapo pande zote zilipinga kesi zao huku Sonko akisisitiza kuwa kuondolewa kwake hakukuafikia vigezo vilivyowekwa chini ya Katiba.

Rufaa hiyo ilisikizwa siku moja tu baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC)kumuidhinisha kuwania kiti cha Gavana wa Mombasa katika uchaguzi wa Agosti.

Mnamo Desemba 3, 2020, Sonko alitimuliwa na Wakilishi wadi 88 wa Bunge la Kaunti ya Nairobi.

Kesi hiyo baadaye ilipelekwa kwa Seneti, kama inavyotakiwa na Katiba mnamo Desemba 17, 2020, ambapo waliidhinisha azimio la kumwondoa afisini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved