logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jacque Maribe akiri kosa la pili

''Sheria iko wazi jinsi taarifa ya washukiwa dhidi ya mwingine inavyochukuliwa'' Hakimu akaamua

image
na

Habari20 July 2022 - 05:43

Muhtasari


•Jacque Maribe aliyeambatana na wakili wake Katwa Kigen anadaiwa kumfungukia Otieno na kumwambia kuwa anataka kubadilisha kauli yake na kusema kilichotokea.

Joseph Irungu akiwa ameshika bunduki ya kivita akiwa na jeraha la risasi. Mfanyabiashara aliyeuawa Monicah Kimani

Joseph Irungu almaarufu Jowie mnamo Jumanne alipoteza ombi la kusimamisha upande wa mashtaka kutoa taarifa ya Jacque Maribe inayomhusisha na kesi ya mauaji.

Jowie, kupitia wakili wake Hassan Nandwa, alikuwa amepinga kutolewa kwa taarifa hiyo iliyoandikwa na Maribe ambapo aliwaambia polisi kwamba yeye (Jowie) alijipiga risasi nyumbani kwake.

Nandwa alisema kauli hiyo ni ya kukiri kosa na inapaswa kuchukuliwa hivyo akimaanisha kwamba taarifa hiyo ilipaswa kufuata utaratibu sahihi wakati inachukuliwa.

Inspekta mkuu Maxwell Otieno alikuwa ameambia mahakama kwamba taarifa aliyochukua kutoka kwa Maribe ilikuwa ya pili kurekodi akiwa na polisi.

Hapo awali Maribe alikuwa amerekodi taarifa yake ya kwanza ambayo ilithibitisha taarifa ya Jowie lakini Septemba 29 aliamua kwa hiari kuibadilisha hivyo kauli ya pili.

Katika uamuzi mfupi, Jaji Grace Nzioka aliruhusu upande wa mashtaka kutoa maelezo ya pili ya Maribe, akisema haitakuwa inatumika  kwa Jowie.

Hakimu Nzioka alisema upande wa mashtaka ulithibitisha kwamba taarifa hiyo haikuwa ya Maribe kama ilivyodaiwa.

 

"Sheria iko wazi jinsi taarifa ya washukiwa dhidi ya mwingine inavyochukuliwa. Hata ikikubaliwa, hatabaguliwa kwani atapata fursa ya kuichunguza,” hakimu akaamua.

Mahakama pia ilisema Maribe, ambaye ndiye mwandishi wa taarifa hiyo, hakuwa amepinga taarifa hiyo kuwasilishwa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved