Taarifa kuhusu usalama huko Molo zinahofia kuwa kuna uwezekano wa makundi haramu kufurushwa katika operesheni zinazoendelea katika maeneo mengine ya mji wa Nakuru huenda yakahamia Mashinani.
Kulingana na Kamishna Msaidizi wa Kaunti Ndogo ya Molo Steve Ondote kuongezeka kwa ukosefu wa usalama katika vijiji vya Mooto na Mutirithia ni jambo la kutisha na kuwahakikishia wakazi wa eneo hilo usalama wao kwani wamejitolea kurejesha usalama katika eneo hilo.
Haya yanajiri wiki moja baada ya msururu wa mashambulizi dhidi ya wakaazi wa vijiji hivyo viwili na magenge yenye silaha, ambapo vyombo vya usalama huko Molo vimekuwa vikiendesha operesheni za ulinzi wa mashirika mbalimbali usiku.
Hapo jana wakaazi kutoka vijiji vya Mutirithia na Miti mirefu walipata fursa ya kutangamana na maafisa wa usalama mjini Molo wakitoa hoja zao kutokana na kukithiri kwa ukosefu wa usalama eneo hilo.
Kulingana na wakazi hao walikubaliana kushiriki na kutoa habari kuhusu kundi hilo la kuhakikisha hatua mwafaka umechukuliwa ya kuhakikisha kesi hizo hazizidi kuongezeka.
Pia wamewataka viongozi wa maeneo hayo kuhakikisha kuwa maeneo mengi kumewekwa taa za barabarani na ufyekaji wa vichaka kando ya barabara ambazo zimebainishwa kuwa chanzo cha kukithiri kwa ukosefu wa usalama.