logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa watano wa genge mjini Kisumu wakamatwa na Polisi

Washukiwa hao walionaswa na kamera ya CCTV waliiba mali ya thamani ya Sh500,000.

image
na

Habari22 July 2022 - 06:29

Muhtasari


•Dennis Odhiambo almaarufu Deno, Hillary Odero almaarufu Konza, Eugene Akello almaarufu Yujo, Alex Amena almaarufu Spanner Boy na Hassan Hussein almaarufu Marwa.

•Polisi wanasema ni wanachama wa kundi la magenge tisa ambalo limekuwa likiwahangaisha wakaazi wa Kisumu.
 

Baadhi ya washukiwa wa genge walikamatwa mjini Kisumu baada ya kudaiwa kuvamia duka la kielektroniki na kuiba bidhaa za thamani ya Sh500,000.

Polisi wamewakamata vijana watano waliosema ni wanachama wa genge la wahalifu mjini Kisumu.

Ni Dennis Odhiambo almaarufu Deno, Hillary Odero almaarufu Konza, Eugene Akello almaarufu Yujo, Alex Amena almaarufu spanner boy na Hassan Hussein almaarufu Marwa.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Kisumu ya Kati Anthony Maina alisema washukiwa hao walivamia duka la vifaa vya elektroniki huko Riat katika kaunti ndogo ya Kisumu Magharibi mnamo Julai 6.

Washukiwa hao walionaswa na kamera ya CCTV waliiba mali ya thamani ya Sh500,000.

Kesi hiyo iliripotiwa katika kituo cha polisi cha Kogony mnamo Julai 8. Duka hilo ni la afisa wa gereza.

Maina alisema walikamatwa Jumatano na maafisa kutoka kituo cha polisi cha Kondele wakiongozwa na OCS Fredrick Kirui.

Watu hao walikamatwa katika mzunguko wa Kondele, Koyango, Molem, Kayengo na Manyatta Arab

Wanashukiwa kuwa wanachama wa kundi la magenge tisa ambalo limekuwa likiwahangaisha wakazi wa Kisumu.

Mkuu huyo wa polisi alisema walikuwa wakiwafuata washukiwa wengine ambao bado hawajashikwa.

Polisi walikamata pikipiki moja ambayo washukiwa wanaodaiwa kutumia wakati wa msako huo.

Washukiwa wengi hutumia pikipiki kutekeleza shughuli zao za uhalifu. Watano hao watahamishiwa katika Kituo cha Polisi cha Maseno, kaunti ndogo ya Kisumu Magharibi kushtakiwa.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved