logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume aliyeteketeza mkewe hadi kufa, ahukumiwa kunyongwa

Tang Lu aligonga vichwa vya habari mwaka 2020 baada ya kurekodi video ya mubashara kwenye TikTok akimchoma mkewe kwa moto hadi kufa.

image
na Radio Jambo

Habari25 July 2022 - 09:05

Muhtasari


• Tang Lu aligonga vichwa vya habari mwaka 2020 baada ya kurekodi video ya mubashara kwenye TikTok akimchoma mkewe kwa moto hadi kufa.

Lamu, mwanamke aliyeteketezwa hadi kufa

Tang Lu, ni mwanaume mmoja raia wa Uchina ambaye mwaka wa 2020 aligonga vichwa vya habari baada ya kumuua mkewe kwa kumteketeza kwa moto hadi kufa huku tukio hilo akilirekodi mubashara kwenye ukurasa wake wa TikTok.

Mwanaume huyo alishikiliwa na kesi yake imekuwa ikiendelea tangu nyakati hizo ambapo wikend iliyopita majarida mbalimbali duniani yaliripoti kwamba hatimaye kesi hiyo imeamliwa kwa mwanaume huyo kuhukumiwa kunyongwa.

Kwa mujibu wa amri ya mahakama ya Watu wa Juu, Tang Lu alinyongwa siku ya Jumamosi baada ya kupewa hukumu ya kifo kwa mauaji ya kukusudia mnamo2020 ambayo yalizua ghadhabu ya kitaifa.

Kulingana na hati ya mahakamani iliyopakiwa na majarida mengi wikendi, mahakama ilisema kwamba tukio alilolifanya kwa mpenzi wake lilikuwa tukio la kinyama na hivyo alistahili adhabu kali kama hiyo ya kunyongwa.

Lu na mkewe Lamu walitengana mnamo Juni 2020 baada ya miaka kumi na moja pamoja. Wote wawili walifanya kazi kama washawishi kwenye Douyin, toleo la Kichina la TikTok.

Kulingana na maelezo ya awali kutoka kwa mahakama, Lu hakuwa tayari kupata talaka na alijaribu mara kwa mara kurejesha ndoa, lakini Lamu alikataa wazo hilo.

Baadqa ya video ile ya kinyama kuonekana kabla ya kufutiliwa mbali na mamlaka ya mtandao huo unakuja kwa kasi za ajabu, kote duniani watu walizua mjadala mkali kuhusu dhuluma na unyanyasaji wa kinyumbani chini ya alama ya reli Lhamo Act huku wakitaka waathiriwa wa visa vya unyanyasaji katika ndoa kuruhusiwa kuchukua talaka na kujiendea zao badala ya kuwafanyia vitendo vya kinyama kama kile cha kuteketezwa moto.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved