logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mrembo alinipenda, wewe wacha domo zege!" Stevo Simple Boy amjibu Rapdon

“Kama kichuna wangu hakupenda Rapdon na kunipenda mimi, hiyo basi akome, anyamaze awache kupiga mdomo zege" - Stevo Simple Boy.

image
na Radio Jambo

Habari01 August 2022 - 11:51

Muhtasari


• Rapdon alijitokeza kudai kwamba Stevo alimchukulia mpenzi wake.

• Stevo alimjibu kwamba kama mrembo alimchagua yeey na kumuacha Rapdon basi huyo jamaa afyate wake ulimi.

Wiki moja baada ya msanii Stevo Simple Boy kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake mpya kwa jina Gee, sasa mwanaume mmoja amejitokeza wazi kusema kwamba Gee alikuwa mchumba wake.

Mwanaume huyo kwa jina Rapdon aliandika kwenye Instagram yake akidokeza kwamba mchumba wa sasa wa Stevo Simple Boy alikuwa ni mchumba wake, huku akidhibitisha kwa kuambatanisha malalamishi hayo kwa picha yao wakiwa wamekumbatiana kabla Simpl Boy hajapindua serikali.

“Tulikuwa tunachumbiana na mchumba wa sasa wa Stevo Simple Boy,” Rapdon aliandika Instagram.

Aidha katika taarifa nyingine zilizofichuliwa na kundi moja la mitandaoni la udaku nchini, mwanaume huyo alielezea kwa kina jinsi matukio yalivyokuwa kabla ya mambo kumuendea mrama ambapo aliamka asubuhi moja tu na kukuta yule aliyekuwa akimuita mchumba wake sasa ni kama shimeji wake.

Alielezea kwamba yeye ni mwanamuziki anayechipukia na alikuwa katika mapenzi na Gee kwa takribani miezi sita ambapo asubuhi moja aliamka akapata mpenzi wake anazungumziwa mitandaoni kwamba Stevo Simple Boy amemchukulia mpenzi wake.

Baada ya madai hayo kumfikia nguli huyo wa Freshi Barida, sasa Simple Boy amejibu madai hayo na kusema kwamba mapenzi si kitu cha kulazimisha bali ni kutu kinakuja chenyewe na kusema kwamab kama Gee hakumpenda Rapdon na kumchagua yeye basi mengine ni ziada tu.

“Kama kichuna wangu hakupenda Rapdon na kunipenda mimi, hiyo basi akome, anyamaze awache kupiga mdomo zege. Mimi kwangu hizo picha na video hazileti vurugu kwa sababu kama mrembo ameshanipenda ndio hivo amenipenda, haina haja ya vita,” Stevo Simple Boy alisema.

Kwa upande wake, Gee alisema kwamba kutokana na video na picha ambazo zimekuwa zikipakiwa na mwanaume huyo, hakuna kikubwa kilichokuwa kikiendelea baina yao na kusema kwamab Rapdon ambaye anadai alikuwa mchumba wake si kweli kwani yeye alikuwa anamchukulia kama ndugu yake.

“Rapdon alikuwa kama kaka yangu na aliamua kupakia hivo nikamwambia azitoe lakini sijui ni kwa nini alikuwa ameamua kufanya hivo,” Gee alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved