logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ngirici amjibu Waiguru baada ya madai ya wizi wa kura Kirinyaga

Ngirici, ambaye anawania kama mgombeaji huru, Jumanne alisema ana imani na zoezi la upigaji kura.

image
na Radio Jambo

Habari10 August 2022 - 17:39

Muhtasari


Ngirici amjibu Waiguru baada ya madai ya wizi wa kura Kirinyaga

Mgombea ugavana wa Kirinyaga Wangui Ngirici amemjibu Gavana wa sasa Anne Waiguru kuhusu madai ya wizi wa kura.

"Mlango pekee wa nyuma ambao tunajua ulikuwa NYS wakati wa umiliki wako. TUPO SITE!" Ngirici alisema katika taarifa siku ya Jumatano.

Waiguru alidai kuwa masanduku mawili ya kura yaliingizwa  katika kituo cha kujumlisha kura cha Kianyaga wakati wa shughuli ya kuhesabu kura.

"Sanduku mbili za kura zilizo na kura ya magavana huingia Kirinyaga kupitia mlango wa nyuma mchana kweupe! LAZIMA ziondolewe na kujumlisha kura lazima kukomeshwa," gavana huyo aliandika.

Waiguru pia alimshutumu Ngirici kwa kupeleka majambazi katika kituo cha kuhesabia kura cha Kianyaga ili "kuvuruga uhesabuji kura."

Ngirici, ambaye anawania kama mgombeaji huru, Jumanne alisema ana imani na zoezi la upigaji kura.

Kujumlisha kura kwa sasa kunaendelea huku nchi ikisubiri kutangazwa rasmi kwa washindi kutoka kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved