logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sean Andrew apakia video ya zamani babu yake Kibaki akisisitiza Amani

“Nataka kuwaambia Wakenya kuwa wavumilivu kwa sababu demokrasia haiwezi kudumu kama hatutavumiliana, unamvumilia rafiki yako, Jirani yako na kuwaacha wawe na maoni tofauti na yako" - Kibaki.

image
na Radio Jambo

Burudani10 August 2022 - 04:58

Muhtasari


• "Haina haja kumuita mtu majina kwa sababu ana haki ya kutoa maoni." - Kibaki.

Mjukuu wa Mwai Kibaki Sean Andrew awasihi wakenya kudumisha amani

Mjukuu wa Mwai Kibaki Sean Andrew amepakia mkanda wa video kwenye instastories zake ambao ni wa marehemu babu yake Rais wa tatu wa Kenya, Mwai Kibaki akiwataka wakenya kuvumiliana haswa kipindi hiki ambapo nchi inajiandaa kutangaziwa rais mpya na viongozi wngine katika nyadhifa zingine tano.

Katika mkanda huo wa video unaomuonyesha Mwai Kibaki enzi za ujana wake, anasikika akiwarai Wakenya kukumbatia amani na kuvumiliana kwa hisia na maoni ya kila mmoja kwani nchi haiwezi kusonga mbele kama watu watatofautiana kisiasa mpaka kufikia kiwango cha kuzushiana fujo.

“Nataka kuwaambia Wakenya kuwa wavumilivu kwa sababu demokrasia haiwezi kudumu kama hatutavumiliana, unamvumilia rafiki yako, Jirani yako na kuwaacha wawe na maoni tofauti na yako, haina haja kumuita mtu majina kwa sababu ana haki ya kutoa maoni. Hiyo ni haki yake ya kimsingi na hakutengenezwa ili kutawalwa kimaoni na wewe wala kuongozwa na wewe” Kibaki anaonekana akizungumza kwenye video hiyo ya kitambo kiasi.

Sean Andrew alizidi mbele kuonesha dhibitisho kwamba alipiga kura yake katika eneo bunge la Westlands Nairobi na kuwasihi wakenya wote mashabiki wake kudumisha amani muda wote.

Andrew ni mjukuu wa rais hayati Mwai Kibaki na alikuwa na ukaribu mkubwa sana na babu yake huyo ambaye wakati wa kifo chake alionekana kudhoofika mno.

Aliivua moja ya pete zake na kuirusha kaburini mwake kama ishara moja ya kumuenzi kwa mapenzi ya dhati kama babu mwema.

Rais Kibaki alihudumu kati ya mwaka 2002 hadi mwaka 2013 kama rais wa tatu wa Kenya kabla ya kustaafu.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved