logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kuapishwa kwa Ruto kutaendelea bila wewe - Gachagua amwambia Uhuru

Mnamo Jumanne, Odinga aliapa kupinga kuchaguliwa kwa Naibu Rais William Ruto.

image
na

Habari17 August 2022 - 19:31

Muhtasari


  • Hii, hata hivyo, itategemea matokeo ya ombi ambalo kinara wa Azimio la Umoja Raila Odinga anapanga kuwasilisha katika Mahakama ya Juu

Kuapishwa kwa rais mpya kutaendelea hata bila kuwepo kwa Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta, Naibu Rais Mteule Rigathi Gachagua amesema.

Hii, hata hivyo, itategemea matokeo ya ombi ambalo kinara wa Azimio la Umoja Raila Odinga anapanga kuwasilisha katika Mahakama ya Juu.

Mnamo Jumanne, Odinga aliapa kupinga kuchaguliwa kwa Naibu Rais William Ruto.

Alipata kura 7,176,141 dhidi ya 6,942,930 za Odinga.

Gachagua ambaye alikuwa akizungumza wakati wa mahojiano kwenye Kass TV alisema kutokuwepo kwake hakutaathiri kwa vyovyote mchakato wa mpito na makabidhiano.

Uhuru amekuwa kwenye rekodi akisema hatakabidhi mamlaka kwa Ruto.

Alitoa mfano wa kisa cha Marekani ambapo rais wa zamani Donald Trump ambaye alishindwa alitoa nafasi kubwa kwa hafla ya kuapishwa kwa kiongozi anayekuja Joe Biden.

“Kinachotakiwa tu wakati wa kuapishwa ni uwepo wa Jaji Mkuu, hata si upanga huo, hiyo ni sherehe tu,” alisema mbunge huyo wa Mathira anayemaliza muda wake.

Aliongeza:

"Lakini tunamwomba awe muungwana."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved