logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+video) "Ali'cheat nikampa adhabu ya kulipia upasuaji wangu wa pua"

"Wakati nilipomkuta akichepuka, nilimwambia kwamba nitaendelea kukaa na yeye ila kwa sharti kwamba asimamie gharama ya upasuaji wa pua yangu"

image
na Radio Jambo

Habari19 August 2022 - 07:19

Muhtasari


• Alidokeza kwamba hata baada ya mchumba wake kulipia gharama ya upasuaji wa pua bado alichepuka tena.

Mwanamke mmoja katika mtandao wa TikTok amezua mjadala mkali mtandaoni kuhusu wapenzi wa kiume wanaochepuka nje ya mahusiano na ndoa kwa kutoa kile alichokitaja kuwa suluhu la kudumu katika suala hilo.

Kulingana na video amabyo aliipakia kwenye mtandao wa TikTok, mwanamke huyo ambaye hata akaunti yake hajaipa jina bali nambari tu anasema kwamba alimfumania mpenziwe akichepuka na mwanamke mwingine na akamkasirikia vibaya.

Mchumba huyo wake aliaibika na kumuuliza ni nini angependa kumfanyia ili hali hiyo isijirudie tena, cha kushangaza ni kwamba mwakamke huyo alimtaka mwanaume wake kumlipia gharama ghali ya kufanyiwa upasuaji wa pua kama fidia ya kuchepuka nje ya mahusiano yao.

“Wakati unamkuta akichepuka na akuulize ungependaakufanyie nini ili kurekebisha hali hiyo,” mwanamke huyo alifuatisha video hiyo kwa maneno hayo.

“Nilifanya hivi wakati nilipomkuta akichepuka, nilimwambia kwamba nitaendelea kukaa na yeye ila kwa sharti kwamba asimamie gharama ya upasuaji wa pua yangu, kitu ambacho nilikuwa nakihitaji kwa muda mrefu. Nilifanya hivi kwa sababu kuchepuka kwake kuliniletea nafsi yangu kukosa amani kabisa na pia kwa sababu sikuwa nataka muda wangu katika mahusiano hayo kuharibiwa tena juu nilifikiria itakuwaje endapo atachepuka tena,” mwanamke huyo alieleza kweney video hiyo fupi.

Mwanamke huyo alifichua kwamba mchumba wake alienda tena akachepuka na sasa kuuliza iwapo gharama hiyo aliyoipata ya upasuaji wa pua kutoka kwake ilikuwa stahiki kwa muda wake kwenye mahusiano yale na kujiridhisha kwamba ndio ilistahiki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved