logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chebukati kuongoza makamishna kutoa heshima za mwisho kwa msimamizi wa uchaguzi aliyeuawa

Marehemu Daniel Musyoka atazikwa katika kijiji cha Muuani, wadi ya Muthetheni, kaunti ndogo ya Mwala.

image
na Radio Jambo

Habari26 August 2022 - 07:00

Muhtasari


•Inatarajiwa kuwa naibu mwenyekiti Juliana Cherera na makamishna Abdi Guliye, Boya Molu, Justus Nyang’aya, Irene Masit na Francis Wanderi pia watahudhuria.

•Musyoka alitoweka mnamo Agosti 11 saa nne kasorobo asubuhi na mwili wake ukapatikana siku nne baadaye huko Mariko, eneo la  Loitoktok, Kaunti ya Kajiado.

Daniel Musyoka

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati Ijumaa ataongoza makamishna sita katika kutoa heshima zao za mwisho kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Embakasi Mashariki Daniel Musyoka.

Inatarajiwa kuwa naibu mwenyekiti Juliana Cherera na makamishna Abdi Guliye, Boya Molu, Justus Nyang’aya, Irene Masit na Francis Wanderi pia watahudhuria.

Kulingana na IEBC, tume hiyo ikijumuisha wafanyikazi wake itakutana mwendo wa saa tatu asubuhi katika Mochari ya Montezuma huko Machakos kisha kuelekea Kijiji cha Muuani, wadi ya Muthetheni, kaunti ndogo ya Mwala kwa mazishi.

Musyoka alitoweka mnamo Agosti 11 saa nne kasorobo asubuhi na mwili wake ukapatikana siku nne baadaye huko Mariko, eneo la  Loitoktok, Kaunti ya Kajiado.

Chebukati aliomba uchunguzi ufanyike haraka kuhusu mauaji na kufunguliwa mashtaka kwa waliohusika.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji alimwagiza Inspekta Jenerali wa Polisi Hilary Mutyambai kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji ya Msimamizi wa Uchaguzi wa IEBC.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved