logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+video) Daddy Owen aeleza sababu ya kuvalia gumboots katika mazishi ya Ngashville

“Nilivalia gumboots sababu nilijua nitashika jembe na koleo la kutupa mchanga wakati wa kumzika rafiki yangu.. nilikuja nimejiandaa." - Owen

image
na Radio Jambo

Habari29 August 2022 - 05:51

Muhtasari


• "Niliimba hata kwa gumboots kwa mara ya kwanza!!! Sote hapa tulimfahamu @ngashtheartist kwa nafasi tofauti,” Owen alifafanua.

Jumamosi ilikuwa ni siku ya kiza kinene cha huzuni na simanzi katika tasnia ya Sanaa ya injili Kenya, katika msiba wa msanii Ngashville.

Daddy owen ambaye amekuwa akimuomboleza Ngash tangu kifo chake kuwekwa wazi wiki jana alionekana kwenye mazishi hayo akiwa amevalia gumboots huku akiwaongoza wasanii wengine na waombolezaji kusherehekea maisha ya Ngash na kumpa buriani.

Owen baadae alifafanua zaidi juu ya uvaaji huu usio wa kawaida kwake haswa kwenye hafla za mazishi na kusema kwamba kuvaa kwake gumboots halikuwa jambo la ghafla bali ni kitu ambacho alifika kwenye msiba akiwa ameratibu akili yake kuhusu matokeo ambayo yangehitaji mkono wake.

Msanii huyo maarufu kwa vibao wa kumtukuza Mungu alisema kwamba ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kuvalia gumboots na kushiriki kutumbuiza kwenye jukwaa.

Pia alisema maana yake kubwa ya kuvaa gumboots ni kwa sababu alikuwa anajua fika angehitajika kushika jembe na kushiriki katika uchimbaji kaburi la kumlaza Ngashville kama njia moja ya kutoa heshima zake za mwisho kwake.

“Nilivalia gumboots sababu nilijua nitashika jembe na koleo la kutupa mchanga wakati wa kumzika rafiki yangu.. nilikuja nimejiandaa. Niliimba hata kwa gumboots kwa mara ya kwanza!!! Sote hapa tulimfahamu @ngashtheartist kwa nafasi tofauti,” Owen alifafanua.

Wasanii wakiongozwa na Daddy Owen walitumbuiza katika msiba huo kwa nguvu zote huku akisema kwamba Ngash alikuwa siku zote ni mtu aliyependa furaha na iliwalazimu kusherehekea maisha yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved