logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo ajiondoa kwenye kinyang'anyiro cha spika

Kiongozi huyo wa Wiper  alikuwa amezimezea mate nyadhifa za spika wa bunge la kitaifa na seneti.

image
na Radio Jambo

Habari07 September 2022 - 05:07

Muhtasari


•Hii ni baada ya kikao cha kitaifa cha chama  cha Wiper kusema azma hiyo itakuwa ya kufedhehesha.

•Wabunge wengi wanaamini kuwa idadi haipendelei muungano wa Azimio- One Kenya ikizingatiwa kwamba baadhi ya wanachama wao wamehamia Kenya Kwanza.

Kiongozi wa Wiper Stephen Kalonzo Musyoka hatawania wadhifa wa spika wa bunge lolote nchini Kenya.

Kulingana na NTV, hatua hiyo ya makamu rais huyo wa zamani ilifuatia baada ya baraza ya chama cha chake cha Wiper kusema kuwa azma hiyo itakuwa ya kufedhehesha.

Jumanne baraza la Wiper lilikutana katika makao makuu ya chama na kumshawishi kiongozi wao kuacha azma yake kuwania uspika na kulenga kujenga jina lake.

Wabunge wengi wanaamini kuwa idadi katika mabunge yote mawili haipendelei muungano wa Azimio- One Kenya ikizingatiwa kwamba baadhi ya wanachama wao wamehamia Kenya Kwanza.

Kiongozi huyo wa Wiper alikuwa amechukua stakabadhi za kutafuta nyadhifa za spika wa Bunge la Kitaifa na seneti.

Katika Seneti, Kalonzo alikuwa miongoni mwa watu 15 ambao walikuwa wamechukua karatasi za uteuzi kwa nafasi ya spika na wawili kwa nafasi ya naibu spika.

Watu wengine ambao wamechukua karatasi hizo kufikia sasa ni Isaac Aluoch, Jared Oundo, George Bush, Dkt Rodgers Manana, Beatrice Kinyua, Dorothy Kemunto na Jecinta Lesiangiki.

Josephat Mutua, Mohamud Halake, Michael Gichuri na Joshua Boit pia walichukuwa karatasi za uteuzi katika Bunge.

Kwa nafasi ya naibu spika, Maseneta wateule Karungo wa Thangwa (Kiambu) na Kathuri Murungi (Meru) walikuwa wamechukua karatasi.

Hata hivyo, kinyang'anyiro hicho kitajulikana baada ya kujua ni nani kati yao atakuwa amerudisha karatasi kufikia Jumatano, saa nane alasiri.

Karatasi za uteuzi zitakazorejeshwa pia zitachunguzwa ili kuhakikisha kuwa wagombeaji wanaafikia vigezo vya sheria.

Maseneta wateule watamchagua spika mara baada ya kuapishwa siku ya Alhamisi.

Miungano yote miwili inapanga vikao vya vikundi vya bunge siku ya Alhamisi wakati bunge la kumi na tatu litafunguliwa.

Baada ya wajumbe wa mabunge yote mawili kuapishwa, utaratibu wa kwanza wa biashara utakuwa ni kuchagua maspika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved