logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Orodha ya viongozi wateule kwenye mabunge ya seneti na la kitaifa

Orodha ya viongozi walioteuliwa kushikilia nyadhifa mbali mbali katika mabunge yote mawili jinsi ilivyochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali.

image
na Radio Jambo

Habari07 September 2022 - 13:33

Muhtasari


• Chama cha ODM kiliwateua Irene Mayaka na John Ngongo kuwakilisha wafanyikazi huku Umulkher Mohamed aliteuliwa kuwakilisha vijana.

Bunge

Serikali imechapisha orodha ya viongozi wote walioteuliwa kushikilia nyadhifa mbali mbali kwenye mabunge ya kitaifa na lile la seneti.

Kutoka chama cha UDA, Jackson Kosgei ameteuliwa kuwakilisha watu wenye ulemavu, Teresia Mwangi kuwakilisha vijana, Abdisirati Ali kuwakilisha kundi la watu waliotengwa, Dorothy Ikiara na Joseph Iraya wakiteuliwa kuwakilisha wafanyikazi kwenye bunge la kitaifa.

Suleka Halum ameteuliwa kuwakilisha wanawake.

Kutoka chama cha ANC, Joseph Denar ameteuliwa kuwakilisha wafanyikazi wa jamii.

Chama cha ODM kiliwateua Irene Mayaka na John Mbadi kuwakilisha wafanyikazi huku Umulkher Mohamed aliteuliwa kuwakilisha vijana.

Jubilee kilimteua aliyekuwa mwakilishi wa kike wa Murang’a Sabina Chege kuwakilisha wanawake huku Wiper wakiwa bado wamezuiliwa kufanya uteuzi kutokana na kesi iliyopo kortini.

Katika orodha ya wanawake walioteuliwa kuwakilisha katika bunge la seneti, chama cha UDA kiliorodhesha Veronica Nduati, Roselinda Tuya, Miraj Abdulrahman, Gloria Orwoba, Joyce Korir, Karen Nyamu, Peris Tobiko, Miriam Omar, na Maureen Mutinda.

Katika kitengo hicho, ODM waliteua Catherine Mumma, Beatrice Oyomo, Hamida Kibwana, Betty Montet, na Beth Syengo. Margaret Kamar aliteuliwa na Jubilee huku Shakilla Mohamed akiteuliwa na Wiper.

Hezena Lemaletian wa ODM na Raphael Mwinzagu wa UDA waliteuliwa Kwenda Seneti kuwakilisha vijana huku Crystal Asige wa ODM na George Mbugua wa UDA wakiteuliwa Kwenda bunge hilo  la seneti kuwakilisha watu wenye ulemavu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved