logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tweet ya mganga akitabiri kifo cha malkia Elizabeth mwaka jana yaibuka "8th Septemba"

“Malkia wa Uingereza atafariki dunia tarehe 8 Septemba. Mimi naona tarehe hii ikimzingira juu ya kichwa chake" mganga aliandika kwenye Twitter mwaka jana.

image
na Radio Jambo

Habari09 September 2022 - 10:10

Muhtasari


• Aliwatahadharisha wale wasioamini katika ushirikina wa Voodoo na kuwaambia wataona.

• Mganga huyo aliandika kweney Tweeter Agosti 24 mwaka 2021 kwamba malkia angefariki tarehe 8 Septemba.

Mganga huyo alibashiri kifo cha malkia Elizabeth wa 2 mwaka jana kulingana na Twitter yake.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya Firauni!

Huku dunia ikizidi kuomboleza kifo cha malkia Elizabeth wa pili kutoka Uingereza, watumizi wa mtandao wa Twitter wameibua Tweet ya mganga mmoja hatari aliyebashiri kifo cha Malkia Elizabeth mwaka mmoja uliopita.

Mganga huyo kupitia Twitter yake amejieleza katika utambulisho wake kwamba yeye ni mtaalamu katika kutoa ubashiri kutumia ushirikina, voodoo.

Malkia alifariki Septemba 8 na Tweet ya huyo mganga kwa jina Orunmila inaonesha kwamab alipiga ramli na kutoa ubashiri wake kuhusu kifo cha Malkia kwamba kingetokea tarehe kama hiyo.

Ubashiri wake unaonekana kwenye Tweeter kutolewa mnamo Agosti 24 mwaka jana.

Baada ya ubashiri huo kutimia kwa kifo cha malkia, sasa Orunmila ametanua kifua na kutamba kwamba kama wewe uko hapo na bado huamini katika uganga wa vood basi umetupa mbao.

“Malkia wa Uingereza atafariki dunia tarehe 8 Septemba. Mimi naona tarehe hii ikimzingira juu ya kichwa chake. Wewe endeleea kutoamini katika voodoo na utaona,” mganga huyo aliandika mwaka jana Agosti kwa lugha ya Kifaransa.

Jana baada ya ubashiri wake kugonga ndipo, mshirikina huyo alirudi kweney Twitter na kujisifu kwamba kazi yake ya voodoo si ya kubahatisha kwani huwa anabashiri na tofauti huwa ni kidogo sana. Alisema kwamab katika ubashiri wake mwaka jana, hangeweza kubashiri sahihi muda na chanzo cha kifo cha malkia Elizabeth.

“Hatuwezi kutenda au kushawishi, kutabiri tu, kujua mapema na wakati mwingine tofuati kidogo kizuri yaa makosa. Hapo sikuweza kujua saa wala sababu ya kifo,” mganga Orunmila aliandika.

Swali ni je, wewe huwa unaamini katika uganga wa kupiga ramli?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved