logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Piki Piki ponk paka mielo disco” Mutula Kilonzo akejeli ombi la kupinga kuchaguliwa kwake

Mutula Kilonzo alionekana kutupilia mbali ombi la mshindani wake Patrick Musimba aliyeelekea mahakamani kupinga ushindi wake.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2022 - 05:16

Muhtasari


• “Hii mpe tu mwanafunzi wa ndani katika kampuni yako ya uwakili ☺️ - hii ni hewa moto,” mmoja kwa jina Gathuki Ngahu alisema.

Gavana wa Makueni apuuzilia mbali kesi ya kupinga ushindi wake.

Gavana wa Makueni Mutula Kilonzo Jr amekejeli ombi lililowasilishwa mahakamani na aliyekuwa mshindani wake katika kinyang’anyiro cha ugavana, Patrick Mweu Musimba.

Musimba alikuwa ni mbunge wa Kibwezi West kabla ya kuingia debeni akilenga kumrithi gavana aliyemaliza hatamu yake ya miaka kumi, profesa Kivutha Kibwana.

Katika barua ya kesi hiyo ambayo iliwasilishwa katika ofisi ya Mutula Kilonzo ikimtaja kama mshtakiwa kwenye kesi hiyo, Musimba pia alitaja tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC.

Katika kile kilichoonekana kama kuipuuzilia mbali kesi hiyo, gavana Kilonzo Jr alipakia barua hiyo na kuifuatisha kwa maneno ya chekechea yaliyotajwa kwenye mahakama ya upeo wiki juzi na wakili Willis Otieno, “Piki Piki ponk paka mielo disco.”

Katika uchaguzi wa Agosti 9, Mutula Kilonzo Jr alipaka kura nyingi mno zaidi ya laki mbili huku Musimba ambaye alikuwa mshindani wake mkuu akipata kura takribani elfu 60 tu, na sasa amewasilisha kesi kupinga kuchaguliwa kwa Kilonzo Jr kwa kile anasema shughuli ya uchaguzi ilikumbwa na dosari chungu nzima.

Baada ya Kilonzo Jr kupakia barua hiyo na kuikejeli kwa maneno ya wakili Willis Otieno, watu wengi walionekana kutolea maoni kwamba Musimba alikuwa anajiabisha bure kwani hata kura alizoshindwa nazo ni nyingi mno.

Wengine walimtaka Kilonzo Jr kuwatuma mawakili wachanga katika kampuni yake ya mawakili ili kumwakilisha kwani kwa hadhi yake hahitaji kabisa kujiwakilisha katika kesi hiyo yenye walisema haina mashiko.

“Hii mpe tu mwanafunzi wa ndani katika kampuni yako ya uwakili ☺️ - hii ni hewa moto,” mmoja kwa jina Gathuki Ngahu alisema.

“Bwana mkuu wa kaunti unaonekana kuonyesha kuwa mlalamishi anajishughulisha na kukimbizana na bata bukini wa mwituni,” Mwalimu Katebes Kibet alitania.

“Nashuka pale nione ni nani huyu anayepuliza hewa moto na kukimbiza bata bukini mwitu huko Makueni, hakuna anayeweza kushindana na Mutula Junior sio Makueni tu bali hata Ukambani. Ngoja tusubiri tuone ataenda wapi,” Charles Kilonzo alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved