logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Balozi wa Kuba amtembelea rais wa NOCK

Tergat alisisitiza haja ya Kenya na Kuba kufanya kazi kwa karibu.

image
na

Habari08 October 2022 - 07:48

Muhtasari


•Tergat alisema kuwa ziara ya balozi huyo inalenga kuhimiza Kenya na Kuba kushirikiana katika programu mbalimbali za michezo.

•Kuba inasifika kwa kutoa baadhi ya mabondia bora zaidi duniani.

Rais wa NOCK, Paul Target akimpokea balozi wa Kuba nchini Kenya Juan Manuel Rodriquez Vazquez, katika afisi yake huko Westlands, Nairobi mnamo Ijumaa.

Kamati ya Kitaifa ya Olimpiki ya Kenya (NOCK) itaendelea kutumia michezo kama njia ya kuanzisha ushirikiano mpya na kuimarisha uhusiano na mataifa mengine.

Rais wa NOCK, Paul Target alisema hayo baada ya kumkaribisha balozi wa Kuba nchini Kenya Juan Manuel Rodriquez Vazquez, katika afisi yake huko Westlands, Nairobi mnamo Ijumaa.

"NOCK inajitahidi kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa kupitia michezo. Tunawahimiza wanariadha wetu kuendeleza uhusiano wa karibu na wenzao kutoka mataifa mengine," Tergat alisema.

Tergat alisisitiza haja ya Kenya na Kuba kufanya kazi kwa karibu, akisema nchi zote mbili zinaweza kufaidika na uhusiano huo wa pande zote.

“Juan Manuel Rodriquez Vazquez, balozi wa Jamhuri ya Kuba leo ametutembelea kwa heshima katika afisi zetu,” Tergat alisema.

Tergat alisema kuwa ziara ya balozi huyo inalenga kuhimiza Kenya na Kuba kushirikiana katika programu mbalimbali za michezo.

"Kuba ina fursa nyingi kwa wanariadha wa Kenya ambao wanaweza kufaidika pakubwa kupitia programu za michezo kati ya nchi hizo mbili.

Kuba inasifika kwa kutoa baadhi ya mabondia bora zaidi duniani.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved