logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chepngetich na Kipruto watwaa mataji ya Chicago Marathon

Kipruto, 31, alimaliza mbio hizo kwa saa 2:04.24 na kurejesha taji alilopoteza Aprili mwaka jana.

image
na

Habari09 October 2022 - 16:58

Muhtasari


•Katika mbio za wanawake, Mkenya Ruth Chepng'etich alihifadhi taji lake.

•Chepng'etich alirekodi muda bora wa binafsi wa 2:14:18, huku akikosa rekodi ya dunia kwa sekunde 14.

Ruth Chepng'etich

Mkenya Benson Kipruto ndiye bingwa wa mwaka huu wa Chicago Marathon baada ya kufutilia mbali safu kali ya washindani kushinda mbio hizo siku ya Jumapili.

Kipruto, 31, alimaliza mbio hizo kwa saa 2:04.24 ili kurejesha taji alilopoteza Aprili mwaka jana.

"Nina furaha kushinda na kuweka PB mpya. pia nina furaha kuweka taji katika familia. Kozi hapa ni tambarare na huu ni mji mzuri," Kipruto alisema baada ya ushindi wake.

Bingwa mtetezi Seif Tura wa Ethiopia alimaliza wa pili kwa 2:04:49 huku bingwa wa Los Angeles Marathon John Korir akimaliza wa tatu kwa 2:05:01.

Katika mbio za wanawake, Mkenya Ruth Chepng'etich alihifadhi taji lake.

Chepng'etich alirekodi muda bora wa binafsi wa 2:14:18, huku akikosa rekodi ya dunia kwa sekunde 14.

Rekodi hiyo iliwekwa na mzalendo Brigid Kosgei kwenye Chicago Marathon mwaka wa 2019.

Emily Sisson wa Marekani alikuwa wa pili kwa saa 2:18:20 huku Vivian Kiplagat akimaliza wa tatu kwa 2:20:52.

Mkenya Bornes Jepkirui alishinda mbio za Lisbon Marathon kwa 2:24:17. Waethiopia Sorome Negash na Buzunesh Getachew walimaliza wa pili na wa tatu kwa 2:25:57 na 2:26:01 mtawalia. Mkenya mwingine Jane Jelagat alimaliza wa saba kwa 2:30:34.

Katika mbio za wanaume, Waethiopia walichukua nafasi tatu za kwanza kupitia Andualem Belay, Haftu Teklu na Birhan Nebew waliotumia saa 2:05:45, 2:06:33 na 2:07:04.

Mkenya Julius Kipkorir alimaliza wa nne kwa 2:08:23. Wakenya wengine katika mbio hizo walikuwa Paul Eyanae na Nicholas Kirwa walioshika nafasi za nane na tisa katika muda wa 2:13:46 na 2:14:31 mtawalia.

Katika mbio za Munich Marathon, Philemon Kipchumba na Agnes Keino walishinda mbio za wanaume na wanawake kwa saa 2:07.28 na 2:23.26 mtawalia.

Mengistu Gezahagn wa Ethiopia na Mueritrea Berhane Tesfay walishika nafasi ya pili na ya tatu nyuma ya Kipchumba katika mbio za wanaume.

Wakenya wengine Edwin Kimaiyo, Rodgers Keror, Meshack Koech na Vincent Kiprotich walimaliza katika nafasi za tano, sita, saba na tisa mtawalia.

Katika mbio za wanawake, Marr Hurssa wa Ethiopia na Souad Kanbouchia wa Morocco walitumia 2:24:12 na 2:27:35 kumaliza wa pili na wa tatu.

Wakenya wengine Viola Yator na Helen Jepkurgat walipata nafasi ya nne na nafasi ya saba baada ya kumaliza kwa muda wa 2:28.11 and 2:32.07 mtawalia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved