logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ujumbe wa mahaba wa Willis Raburu kwa mpenziwe anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa

Mtangazaji huyo wa runinga alisema anajivunia mchumba wake

image
na Radio Jambo

Habari17 October 2022 - 13:27

Muhtasari


  • Willis na mpenzi wake Ivy wamebarikiwa na watoto wawili, huku wawili hao wakiwasherehekea watoto wao

Mtangazaji Willis Raburu ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao wanafahamika sana mitandaoni kutokana na kazi yao na maisha yao binafsi

Willis na mpenzi wake Ivy wamebarikiwa na watoto wawili, huku wawili hao wakiwasherehekea watoto wao.

Huku akimlimbikizia sifa akisherehekea siku yakke ya kuzaliwa, Willis alimshukuru kwa kubadilisha maisha yake.

Katika ujumbe wake, Willis alieleza Namu kama mwanamke mkuu ambaye alileta amani si kwake tu bali kwa familia yake na marafiki pia.

Mtangazaji huyo wa runinga alisema anajivunia mchumba wake akibainisha kuwa hana chochote ila kumpenda.

“Namu wangu Tamu! Heri ya siku ya kuzaliwa nyota yangu! Mchumba wangu, Wewe ni moyo wa kweli, roho ya kweli na roho iliyotulia. Nuru yako huangaza hata nyakati za giza za dakika na unaleta amani na upendo mwingi kwangu na familia na marafiki zetu.

Ninajivunia wewe, ninakusherehekea na kumshukuru Mungu kwa ajili yako. Shine on! HAPPY BIRTHDAY! Ninakupenda sana," Willis aliandika.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved