logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mfahamu binadamu mwenye macho makubwa zaidi duniani

Sidney de Carvalho Mesquita  anaripotiwa kuwa na macho yenye mduara wa milimita 18.2.

image
na Radio Jambo

Habari27 October 2022 - 09:21

Muhtasari


• Sidney de Carvalho Mesquita almaarufu Tio Chico kutoka Brazil anashikilia rekodi ya ulimwengu ya binadamu mwenye macho makubwa sana.

•Sidney alisema hapo awali familia yake ilikuwa na wasiwasi kuwa huenda ni ugonjwa.

​​Sidney de Carvalho Mesquita

Nani angewahi kufikiria kwamba mtu angeingia kwenye Kitabu cha Rekodi za Dunia kwa kuwa na macho makubwa?

Jamaa mmoja anayejulikana kama Sidney de Carvalho Mesquita almaarufu Tio Chico kutoka Brazil anashikilia rekodi ya ulimwengu ya binadamu mwenye macho makubwa sana.

Inaaminika macho yake ina mduara wa milimita 18.2, takriban inchi 0.71 tofauti na macho ya binadamu wa kawaida, hali ambayo inaweza kumfanya kuyatoa macho yake nje  umbali wa takriban sentimita  mbili.

Inaripotiwa kuwa kadri muda unavyosonga ndivyo macho ya Tio Chico yanazidi kuwa makubwa zaidi na kuchomoza zaidi kuliko  ya wanadamu wenzake, jambo ambalo familia yake na marafiki wameshangazwa nalo.

Alipohojiwa, Tio Chico alifichua kuwa wakati ambapo ameyakondoa macho kisha kuyarudisha ndani huwa anapoteza uwezo wa kuona kwa sekunde kadhaa. Aidha alfichua aligundua ana mboni kubwa ya macho kuliko kawaida, akiwa na umri mdogo wa miaka tisa  alipokuwa akijitazama kwenye kioo.

Sidney alisema hapo awali familia yake ilikuwa na wasiwasi kuwa huenda ni ugonjwa, ila baadaye walikuja kukubali na kusema hali yake ilikuwa ujuzi wa kipekee.

"Talanta yangu hakika ni zawadi niliyopewa na anaifurahia." alisema.

Anasema anashukuru kwa hali aliyozaliwa nayo kwani ilimletea sifa na kumfanya kutambuliwa sio tu nchini Brazil bali ulimwenguni kote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved