logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Felicity avunja kimya baada ya Andrew Kibe kuwauliza wafanye DNA

Felicity alibarikiwa na mtoto wake  Zoey tarehe 4/11/2022.

image
na Radio Jambo

Habari09 November 2022 - 14:50

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram kwenye, kipindi cha maswali na majibu, mmoja wa mashabiki wake alimuuliza iwapo watafanya vile Kibe alikuwa amewauliza

Muunda maudhui Felicity Shiru, amevunja kimya baada ya mtangazaji Andrew Kibe kuwauliza wafanye DNA ya mtoto wao na mpenzi wake Thee Pluto.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram kwenye, kipindi cha maswali na majibu, mmoja wa mashabiki wake alimuuliza iwapo watafanya vile Kibe alikuwa amewauliza.

"Kibe alisema mfanye DNA mtafanya kweli?"Shabiki aliuliza.

Huku akijibu swali hilo mama wa mtoto mmoja alisema kwamba hataki kuongea vibaya kutokana na usemi wake Kibe.

"Acha nisongee vibaya,"Alijibu Felicity.

Felicity alibarikiwa na mtoto wake  Zoey tarehe 4/11/2022.

Thee Pluto akisherehekea kuzaliwa kwa mwanawe alimnakili ujumbe wa kipekee,huku akimjulisha kwamba ametimiza ndoto yake.

Aliendelea na kumshukuru mwanawe, kwa kumbadilisha na kufanya aitwe baba,na kupewa heshima.

"Nimetimiza ndoto zangu kwa kumpata mwanangu. Karibu duniani mtoto wangu @zoey_pluto Umenibadilishia jina nikawa mzazi na ukanipa heshima. Nakuombea Maisha mema. My true love ❤️,"Aliandika Pluto.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved