logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Anne Waiguru akutana na Bill Gates amsawishi kufadhili miradi muhimu

Bill Gates pia alizuru Kaunti ya Makueni ambapo alifanya mkutano na gavana wa eneo hilo.

image
na Radio Jambo

Habari17 November 2022 - 13:46

Muhtasari


  • Mkutano huo ulikuwa sehemu ya ziara ya Bill Gates nchini Kenya. Aliwasili nchini Jumanne, Novemba 15 kwa ziara ya wiki moja

Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru mnamo Alhamisi, Novemba 17, aliupongeza Wakfu wa Bill Gates kwa msaada katika uboreshaji wa huduma za afya kwa Wakenya.

Waiguru, ambaye alizungumza wakati wa mkutano kati ya Baraza la Magavana na Wakfu wa Bill Gates alibainisha kuwa machifu wa kaunti walijitolea kutekeleza mpango wa Huduma ya Afya kwa Wote.

Hata hivyo, alitoa wito wa kuungwa mkono katika mipango hiyo ili kuhakikisha kuwa mpango huo unanufaisha watu katika ngazi ya kaunti.

Huku akiangazia mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya afya tangu kuja kwa ugatuzi, Waiguru alibainisha kuwa kuongezwa zaidi kwa huduma za afya kwa jamii kutasaidia katika kupunguza changamoto za kiafya.

Waiguru pia aliangazia mimba za utotoni kuwa kero kuu kwa magavana na kuomba ushirikiano kutoka kwa Wakfu wa Bill Gates ili kuhakikisha kuwa vijana walioathiriwa wanapata nafasi ya kurejea masomo yao.

"Aliomba kuungwa mkono katika programu za utetezi wa Afya ya Uzazi ili kupunguza mimba za mapema  pamoja na msaada katika uanzishwaji wa nyumba za kulelea watoto ambapo kina mama vijana wanaweza kuwaacha watoto wao wakitafuta elimu."

Maeneo mengine ya uwezekano wa ushirikiano yaliyosisitizwa na Gavana ni pamoja na kuwajengea uwezo wafanyakazi wa kujitolea wa afya ya jamii, wakunga wa jadi na kupitia teknolojia kama vile uchunguzi wa ultrasound na matumizi ya akili bandia.

Mkutano huo ulikuwa sehemu ya ziara ya Bill Gates nchini Kenya. Aliwasili nchini Jumanne, Novemba 15 kwa ziara ya wiki moja.

Mkubwa huyo wa biashara wa Marekani alikutana na Rais William Ruto na wakakubaliana kushirikiana katika maendeleo ya sekta mbalimbali.

Bill Gates pia alizuru Kaunti ya Makueni ambapo alifanya mkutano na gavana wa eneo hilo.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved