logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diana Marua ampongeza Bahati kwa kuwa baba anayejitahidi

Marua alisema kuwa Bahti amemsaidia kwenye malezin ya watoto wao

image
na Radio Jambo

Habari18 November 2022 - 11:45

Muhtasari


• Marua alisema kuwa Bahati amejishindia mapendeleo ya watoto wao kwani chochote wanachohitaji au kuitisha wanapewa.

Diana Marua amemshukuru mume wake Bahati kwa kuwa baba anayejitahidi kuwalea wanao.

Kwenye Instagram, Diana alimwandikia mume wake ujumbe huku akieleza jinsi alivyojitahidi kuwa baba mzuri.

"Siwezi kutaka kuwa na kitu kingine chochote ila wewe kuwa baba ya watoto wangu. Kama kuna mtu ambaye watoto wetu wanafurahia kuwa karibu nao ni wewe," Marua alisema.

Alisema kuwa Bahati amepata upendo wa watoto kwani chochote wanachohitaji au kuitisha wanapewa.

Jambo hilo limefanya Marua kuwa mzazi anayejulikana kuwa mkali na watoto wake.

"Asante kwa kunifanya kuonekana kuwa mzazi 'mbaya' wakati mwingine. Hakuna peremende kwa nyumba na nimenena! Tunakupenda baba yetu Bahati Kenya," aliandika.

Wawili hao walimpokea mtoto wao wa kike hivi majuzi na mwanamuziki huyo amekuwa akijikakamua kumsaidia Marua kumlea.

Bahati amekuwa akipakia picha akimlea mtoto wake mchanga.

"Wakati mwingine nikihitaji miujiza, ninamwangalia binti yangu machoni kisha nafahamu kuwa nina miujiza tayari!" Bahati aliandika huku kwenye picha akimbusu binti yake.

Hivi majuzi, wanandoa hao walitangaza kuzaliwa kwa binti yao Jumanne tarehe 1 mwezi wa Novemba na kumpa jina Malakia Nyambura Bahati.

Wawili hao walipokea jumbe za heri njema mitandaoni kutoka kwa mashabiki wao wakiwemo watu mashuhuri.

Marua alikuwa amesubiriwa kwa hamu na mashabiki wake kujifungua huku wengine wakishuku kuwa alijifungua kitambo na alikuwa akitafuta kiki.

Bahati pia amekuwa akitumia wakati wake kuwalea watoto wake wengine Majesty na Heaven akiwafunza mambo kama kucheza piano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved