logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Samahani-Aisha Jumwa aomba radhi baada ya kumtambua Rais Ruto kama 'Naibu Rais'

Baada ya matamshi yake Jumwa Rais Pia alionekana akiangua kicheko.

image
na Radio Jambo

Habari18 November 2022 - 12:47

Muhtasari


  • Jumwa hakuwa mwepesi kuomba msamaha akisema kuteleza kwake ulimi ni kwa sababu alizoea kumwita Ruto, Naibu Rais kwa muda mrefu

Kulikuwa na nyakati za kufurahisha wakati wa hafla ya kuzindua kiwanda cha Devki Steel Mills, kiwanda hicho kilizindduliwa na Rais William Ruto siku ya Ijumaa.

Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Utumishi wa Umma na Jinsia Aisha Jumwa aliwaacha watazamaji wakiwa wameduwaa baada ya kumtambua Ruto kama Naibu Rais.

"Mimi nataka nichukue nafasi hii kwanza kabisa nimshukuru Naibu wa...," alinyamaza huku wananchi wakiangua kicheko

Baada ya matamshi yake Jumwa Rais Pia alionekana akiangua kicheko.

Jumwa hakuwa mwepesi kuomba msamaha akisema kuteleza kwake ulimi ni kwa sababu alizoea kumwita Ruto, Naibu Rais kwa muda mrefu.

"Samahani, kunradhi, tumeishi naye kama naibu wa rais sana," alisema.

Alimshukuru Ruto kwa kumpa nafasi ya kuhudumu katika Baraza la Mawaziri.

"Ningependa kuchukua fursa hii kumshukuru rais kwa kunichagua kuwa waziri katika Baraza la Mawaziri," alisema.

Ni heshima kubwa kuwa amewapa wananchi wa Pwani fursa, ingawa mimi si waziri wa pwani, mimi ni waziri wa Kenya, nilipochukua kiapo nilichoapa kuwa Waziri Mkuu wa nchi nzima."

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved