logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Miguna Miguna amsuta Bobi Wine kwa kulinganisha Kenya na Uganda

"Nilishangazwa wakati wa uchaguzi wa Kenya kwamba mtandao ulikuwa bado unaendelea

image
na Radio Jambo

Habari19 November 2022 - 06:08

Muhtasari


  • Miguna alitaja mauaji ya maafisa wa IEBC na kushambuliwa kwa makamishna wa IEBC siku ambayo matokeo ya uchaguzi yalikuwa yakitangazwa
Miguna Miguna

Wakili Miguna Miguna amemsuta na kiongozi wa upinzani nchini Uganda Bobi Wine kwa kulinganisha Kenya na Uganda.

Bobi Wine ambaye alikuwa kwenye mahojiano katika kituo kimoja cha runinga nchini aliipongeza Kenya kwa kufanya uchaguzi wa amani hata kama alionekana kumkosoa rais wa Uganda Yoweri Museveni kwa kutoruhusu uchaguzi huo katika nchi jirani.

"Nilishangazwa wakati wa uchaguzi wa Kenya kwamba mtandao ulikuwa bado unaendelea, sikuona watu wakitekwa nyara au kuwepo kijeshi. Sikuona wapinzani wa aliyekuwa madarakani. chini ya kizuizi cha nyumbani," Bobi Wine alisema katika mahojiano siku ya Alhamisi.

Huku akimjibu, Miguna alipuuzilia mbali dhana hiyo akisema Kenya ilikumbwa na vitendo haramu wakati wa uchaguzi wa Agosti 9.

Miguna alitaja mauaji ya maafisa wa IEBC na kushambuliwa kwa makamishna wa IEBC siku ambayo matokeo ya uchaguzi yalikuwa yakitangazwa.

"Wakenya wasio na hatia walitekwa nyara, kutishiwa na kunyanyaswa, wakiwemo maafisa wawili wa IEBC waliouwawa. Mwenyekiti wa IEBC na makamishna wawili walishambuliwa kimwili katika Bomas of Kenya. Acha ulinganisho huu wa kipumbavu kati ya Kenya na Uganda!"

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved