logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Daktari bandia Mugo Wairimu ahukumiwa miaka 29 jela

Mugo amehukumiwa miaka 29 na miezi sita kwa kosa la kuwadhulumu wanawake kingono.

image
na Radio Jambo

Habari21 November 2022 - 09:44

Muhtasari


• Hakimu Wendy Muchemi alisema Mugo ni hatari kwa jamii, hivyo anafaa kuwekwa pembeni kwa muda mrefu.

Daktari bandia Mugo wa Wairimu amehukumiwa kifungo cha miaka 29 na miezi sita jela baada ya kupatikana na hatia ya kuendesha kliniki kinyume cha sheria na kuwapa wagonjwa dawa za kulevya ili kuwadhulumu kingono.

Hakimu Wendy Muchemi alisema Mugo ni hatari kwa jamii, kwa hivyo anafaa kuwekwa mbali na jamii kwa muda mrefu.

"Yeye ni hatari kwa jamii badala ya kutumia ujuzi anaosema aliupata kuboresha jamii aliendelea kwa kujidai kuwa daktari wa wanawake na kuwapa dawa na kuwadhulumu," hakimu huyo alisema katika uamuzi wake.

Mugo alipatikana na hatia ya kuendesha kliniki kinyume cha sheria na kuwapa wagonjwa dawa za kulevya ili kuwadhulumu kingono.

Alisema Mugo aliamua kutumia vibaya ujuzi wake aliohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi kuwapa wagonjwa dawa kwa kuwapa wagonjwa wa kikie dawa za usingizi na kuwadhulumu kingono.

Katika utetezi wake, Mugo alisema alijuta kwa kuanzisha juhudi za za kutumikia jamii na nchi lakini anajuta kwa kuwa sasa yuko gerezani.

Mugo tayari anatumikia kifungo cha miaka 11 jela kwa kuendesha vituo vya matibabu visivyo na leseni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved