logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond asema hata yeye haelewi ni kwa nini kila siku anazidi kupungua uzito wa mwili

Halafu nimekuwa mdogo, kila siku nazidi kuwa mdogodogo. Hilo swala linawachanganya Watanzania wengi - Diamond.

image
na Radio Jambo

Habari21 November 2022 - 12:38

Muhtasari


• Mbosso alimtania kuwa kupoteza kwake uzito wa mwili kunamfanya aonekane kama hana miaka 40 kwenda juu.

Diamond azidi kuingiwa na shaka kupoteza uzito wa mwili wake

Diamond kwa mara ya kwanza amezunumzia mwonekano wa mwili wake na kusema kuwa hata yeye haelewi ni kwa nini kila siku anazidi kupungua.

Akiandika katika moja ya picha ambazo Mbosso alipakia kwenye ukurasa wake wa Instagram, Diamond alionesha kushangaa kwake kutokana na kuendelea kupunguka kwa mwili wake na kila siku kuonekana kama kitoto.

Alisema kuwa si yeye tu anazidi kushangaa kutokana na mabadiliko hayo ya mwili wake bali pia hata Watanzania wote wamekuwa wakiibua maswali kama hayo.

“Halafu nimekuwa mdogo, kila siku nazidi kuwa mdogodogo. Hilo swala linawachanganya Watanzania wengi,” Diamond aliandika.

Jibu la Mbosso ndio liliwaacha wengi katika gumzo kubwa kwani walionekana kutolielewa.

Kwa kawaida wengi wanamjua Diamond kuwa wa miaka chini ya arobaini lakini kwa jibu la Mbosso alionekana kudokeza kuwa msanii huyo tajiri wa WCB Wasafi ana miaka zaidi ya 40 hivi.

“Kweli kaka kama hauna miaka 40 vile safi Sanaa,” Mbosso aijibu na kuwaacha wengi kweneye mataa.

Kama unatilia shaka kuhusu kupungua kwa uzito wa mwili wa Diamond Platnumz, ingia kweney kurasa za mitandao yake ya kijamii na upate kutathmini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved