logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ahsante kwa kuwa baba mwema kwa mtoto wetu - Nadia amwambia Arrow bwoy

Nadia Mukami alisema kuwa Arrow Boy amekuwa akimsaidia katika malezi ya mtoto wao

image
na Radio Jambo

Habari22 November 2022 - 04:38

Muhtasari


• Kwenye Instagram Mukami alipakia video akimshukuru Arrow Boy kwa kuwa baba mzuri kwa mtoto wao.

• Mtoto wa wapenzi hao, Kai ambaye ni wa kiume amefikisha takriban miezi minane sasa tangu kuzaliwa.

Mwanamuziki Nadia Mukami alimwandikia mpenzi wake Arrow Boy ujumbe huku akimsherehekea siku ya wanaume duniani.

Kwenye Instagram Mukami alipakia video akimshukuru mwanamuziki huyo kwa kuwa baba mzuri kwa mtoto wao.

"Kwa baba ya mtoto wangu almaarufu mpenzi wangu wa maisha ambaye hunisaidia kumlea mtoto wetu, Kai 22/7 haswa asubui kwa kuwa mimi si mtu wa kuamka mapema kabisa !! Asante," Nadia aliandika.

Nadia alizidi kumtakia mpenzi wake mema na kumpongeza kwa uwajibikaji wake.

Mtoto wa wapenzi hao wawili, Kai ambaye ni wa kiume amefikisha takriban miezi minane sasa tangu kuzaliwa.

Hivi majuzi, Mukami alipakia video ya kusherehekea mwanawe alipokuwa anafikisha miezi sita.

Alikuwa akicheza kwa mbwe mbwe huku Kai akiwa amefungwa kifuani mwake.

Mama huyo wa mtoto mmoja alikuwa anacheza kwa wimbo wake mpya ambao aliutoa mwezi wa Septemba akimshirikisha mpenzi wake Arrow Bwoy, wimbo kwa jina Kai Wangu.

“Mr Handsome ana miezi 6 😌♥️ Tuliamua kwenda kusherehekea nje ya Nairobi♥️🌺 Nakupenda sana mtoto wangu Kai, wewe ni furaha yangu na najivunia kuwa mama yako,” Nadia Mukami aliandika kwenye video hiyo.

Hivi majuzi Arrow Boy alikuwa anamsherehekea Nadia kwa siku yake ya kuzaliwa ambapo alimwandikia ujumbe.

"Ukaribu wetu unazidi Kuimarika Kila Siku. Mama wa ajabu kwa mwana wetu, mpenzi wa ajabu na rafiki , @nadia_mukami Nampenda mwanamke ambaye umekuwa ... Mwenyezi akujalie Kila la heri unapofikisha miaka 23 😁 heri njema ya kuzaliwa malkia wangu nakupenda," Arrow Bwoy alisema.

Wawili hao wamekuwa wakichumbiana kwa muda sasa baada ya Arrow Boy kumvalisha mama huyo pete ya uchumba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved