logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wabunge watishia kuwasilisha hoja ya kumbandua waziri Moses Kuria

Mbunge wa Pokot Kusini David Pkosing alisema kuwa watakusanya sahihi kuanzia Jumatano

image
na Radio Jambo

Habari22 November 2022 - 11:47

Muhtasari


  • Mbunge wa Pokot Kusini David Pkosing alisema kuwa watakusanya sahihi kuanzia Jumatano wakitaka kumbandua Kuria ikiwa hatabadilisha msimamo

Baadhi ya Wabunge wa Bonde la Ufa wametishia kuwasilisha hoja ya kumbandua Waziri wa Biashara Moses Kuria kuhusu uamuzi wa kuruhusu kuingizwa nchini kwa mahindi ya GMO.

Wakihutubia wanahabari Jumanne, wabunge hao wakiongozwa na Seneta wa Nandi Samson Cherargei walipinga uagizaji wa mahindi kutoka nje ya nchi, wakitaka wizara ya Biashara isitishe mchakato huo mara moja.

"Kama wabunge kutoka mikoa inayopanda mahindi, tunataka kujua ni kwa nini meli tayari zinatia nanga katika Bandari ya Mombasa bila taratibu zilizowekwa," Cherargei alisema. .

Mbunge wa Pokot Kusini David Pkosing alisema kuwa watakusanya sahihi kuanzia Jumatano wakitaka kumbandua Kuria ikiwa hatabadilisha msimamo.

"Atakuwa Katibu wa kwanza wa Baraza la Mawaziri kuondoka madarakani. Tutambandua Tutakusanya saini ikiwa hatabadilika," alisema.

Waziri wa Biashara Moses Kuria alisema Jumatatu kuwa notisi ya kisheria ya kuingizwa nchini kwa Mahindi Yaliyobadilishwa Jeni na wasagaji ilitolewa wiki hii.

Hata hivyo, kabla ya Serikali kutoa mamlaka ya kisheria ya kuagiza mahindi kutoka nje ya nchi, Meli hiyo ilitia nanga katika Bandari ya Mombasa.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved