logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alikuwa amelewa-Willy Paul aweka mambo bayana baada ya Jovial kudai si mpenzi wake

Sababu zake ni kwamba hakuweza kustahimili joto kichwani kutoka kwa mashabiki tena.

image
na Radio Jambo

Habari01 December 2022 - 11:51

Muhtasari


  • Alisema kuwa Willy Paul na yeye walikuwa wanafanya kazi kwenye mradi ambao walimaliza na kuachana

Msanii Jovial amevuma sana mitandaoni baada ya kudai kwamba yeye sio mpenzi wake msanii Willy Paul.

 Sababu zake ni kwamba hakuweza kustahimili joto kichwani kutoka kwa mashabiki tena.

Alisema kuwa Willy Paul na yeye walikuwa wanafanya kazi kwenye mradi ambao walimaliza na kuachana.

Kwa hivyo, ukaribu huo uliofichwa ulikusudiwa kuvuta hisia za mashabiki wao walipotoa wimbo mpya uliopewa jina La la la.

Hata hivyo ametaja kuwa wote wawili walinufaika kutokana na kile walichokifanya, jambo ambalo lilifanya mitandao ya kijamii kuwa mbaya

"Pooze sio mwanamume wangu, ni rafiki yangu ilikuwa biashara na tunufiaka sisi sote, sasa turudi kwenye ukweli, naumia nimeshindwa kuvumilia 

Mungu nisaidie kwa yatakyo fwata, mayooo," Jovial Aliandika.

Huku Willy Paul akijibu madai ya Jovial alisema kwamba alikuwa amelewa na kwamba msanii huyo ni mpenzi wake.

"Tafadhali msitilia maanani uvumi huo, alikuwa amelewa aliposema hayo.. @jovial_ke mambo ya nyumbani tumalize nyumbani please 🙏,"Alisema Willy Paul.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved