logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume akimbia uchi kwenda kambi ya jeshi la KDF Kilifi, apigwa risasi hadi kufa

Iliarifiwa mwanaume huyo alishauriwa kukimbia uchi ili kumzubaisha mlinzi na kutekeleza wizi.

image
na Radio Jambo

Habari11 December 2022 - 07:12

Muhtasari


• KDF walijaribu kumtia woga kwa kufyatua risasi hewani lakini alizidi kutia jitihada za kuingia kambini.

• Alifyatuliwa risasi shingoni na kuuawa papo hapo.

Kielelezo

Kioja kilishuhiwa katika kaunti ya Kilifi kwenye kambi ya jeshi la KDF ya Mariakani baada ya mwanaume aliyekuwa akikimbia uchi kupigwa risasi na afisa wa KDF na kufariki papo hapo.

Kulingana na taarifa, mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 25 alisemekana kushauriwa na mganga wa kienyeji kukimbia uchi kwenda kambi hiyo ya jeshi.

Licha ya afisa wa KDF aliyekuwa amelinda lango la kambi ya jeshi ya Mariakani kupiga risasi hewani ili kumtia woga asiingie, mwanaume huyo kwa jina Juma Kitsao Kombe alikuwa amejitahidi kuingia kwa fujo ndipo afisa akamfyatulia risasi shingoni na kumuua.

Jarida la The Star liliripoti kuwa Kombe alitambuliwa na mama yake. Marehemu anasemekana kuwa miongoni mwa genge ambalo limekuwa likiwahangaisha wenyeji wanaopakana na kambi hiyo.

Aliambiwa kuwa akiwa hana nguo angeweza kumfanya mlinzi huyo alale na hivyo angeondokana na nyara yoyote ambayo angeiba kambini.

Polisi walisema wanachunguza kesi hiyo. Wapelelezi kutoka Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) waliotembelea eneo la tukio walipata katuni mbili zilizotumika ambazo zitafanyiwa uchunguzi wa kina.

Mwili wa marehemu ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali Kuu ya Pwani ukisubiri uchunguzi wa maiti.

Wakaazi wa kaunti ya Kilifi baadhi wanaamini sana katika masuala ya kishirikina, uganga na uchawi ambapo katika miaka ya nyuma visa vya watu wazee kuuawa na watoto wao kwa kushukiwa kuwa wachawi vimekuwa vikiripotiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved