logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu pesa ambazo Argentina itapeleka nyumbani baada ya kushinda Kombe la Dunia

Mashindano hayo yalikamilika rasmi siku ya Jumapili huku Argentina ikiibuka kuwa mshindi.

image
na

Habari19 December 2022 - 06:25

Muhtasari


•Mabingwa washindi watapata kitita cha dola milioni 42 (Ksh5.186 bilioni ) huku washindi wa pili watkipata $30m (Sh3.70 bilioni).

•Timu nyingine 16 zilizoshindwa katika hatua ya makundi zitapokea kwa usawa Sh1.11 bilioni.

Mashindano ya Kombe la Dunia mwaka wa 2022 yalikamilika rasmi siku ya Jumapili huku timu ya taifa ya Argentina ikiibuka kuwa mshindi.

Mashindano hayo yanayotazamwa kote duniani yalishuhudia Argentina ikishinda kwa mabao 4 dhidi ya Ufaransa ambao walifanikiwa kufunga penalti mbili pekee

Kabla ya mikwaju ya penalti, mechi hiyo ilikuwa imekamilika kwa sare ya 3-3.

Mabingwa washindi watapata kitita cha dola milioni 42 (Ksh5.186 bilioni ) huku washindi wa pili watkipata $30m (Sh3.70 bilioni).

Katika kipindi cha kwanza, nyota wa Argentina, Lionel Messi na Angel Di Maria waliiweka timu hiyo ya Amerika Kusini kifua mbele kwa mabao 2-0.

Hii ilikuwa baada ya Messi kupiga mkwaju wa penalti dhidi ya Ufaransa.

Alifunga penalti hiyo dakika ya 23.

Kipindi cha pili, Wafaransa walikuja wakiwa tayari kwa mechi hiyo, huku Kolo Muani akiwashindia penalti sawa na ile aliyopewa Messi.

Penati hiyo ilifungwa na mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe.

Mbappe pia alifunga bao la pili na kuifanya timu ya Ufaransa kupata sare.

Croatia, ambao walimaliza wa tatu dhidi ya Morocco Jumamosi watapewa dola 27m (Sh3.32 bilioni) huku Atlas Lions wa Morocco wakinyakua hadi $25m (Sh3.08 bilioni) kwa kumaliza nafasi ya nne.

Timu nne zilizopoteza katika hatua ya robo fainali zitapata $17m (Sh2.09 bilioni) huku $13m (Sh1.60 bilioni) zikitolewa kwa timu nane zilizoshindwa katika 16 bora.

Timu nyingine 16 zilizoshindwa katika hatua ya makundi zitapokea kwa usawa Sh1.11 bilioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved