Kylian Mbappe ametangaza kwamba watarejea kwa ukubwa na bora zaidi katika Kombe la Dunia la 2026.
Timu ya Mbappe ilishika nafasi ya pili baada ya Argentina kuifunga Ufaransa 4-2 kwa mikwaju ya penalti baada ya sare ya 3-3 katika muda wa nyongeza.
"Nous reviendrons," Mbappe alisema. Maana yake, "Tutarudi!"
Mshambuliaji wa Ufranasa ataondoka Qatar kama mfungaji bora zaidi wa shindano baada ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao matatu katika fainali ya Kombe la dunia tangu alipofunga mabao hayo Geoff Hurst mwaka 1966 -lakini kumbukumbu yake kuu itakuwa ni machungu ya kushindwa.
Baada ya mwisho wa mechi ya kusisimua kusema kweli , Mbappe mwenye umri wa miaka 23 bado aliweza kupanda kwenye jukwaa la ushindi kuchukua tuzo lake binafsi baada ya kuionyesha dunia kipaji chake kikubwa katika soka – lakini kulikuwa na kipindi ambapo ilionekana kuwa alikaribia kupata zawadi kubwa zaidi.
Nous reviendrons. 🇫🇷🙏🏽 pic.twitter.com/Ni2WhO6Tgd
— Kylian Mbappé (@KMbappe) December 19, 2022
Hii ingekuwa fainali yake, na kufahamika kama shindano lake pia, lakini kwa yeyote haya yote atakumbukwa mchezaji mwingine nambari 10, ambaye pia alinyenyua Kombe la Dunia, ambalo Mbappe alilipeleka nyumbani miaka minne iliyopita.