logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanasoka wa Senegal wakasirishwa na marupurupu ya Kombe la Dunia

‘’Ukishinda lazima utazawadiwa, lakini ukishindwa lazima ujifunze kutokana na hilo,’

image
na Radio Jambo

Habari22 December 2022 - 15:51

Muhtasari


  • Mabingwa hao wa Afrika walikuwa wamepewa jukumu la kutinga robo-fainali lakini walitinga katika raundi ya pili

Uamuzi wa Rais Macky Sall wa kukipa kikosi cha soka cha Senegal marupurupu yake ya Kombe la Dunia licha ya timu hiyo kutofikia lengo lake umezua hasira kwa baadhi ya watu katika taifa hilo la Afrika Magharibi.

Mabingwa hao wa Afrika walikuwa wamepewa jukumu la kutinga robo-fainali lakini walitinga katika raundi ya pili baada ya kushindwa 3-0 na Uingereza.

‘’Tutalipa kikamilifu marupurupu ya kufuzu kwa robo-fainali kwa ujumbe wote rasmi,’’ Sall alitangaza siku mbili baadaye.

Marupurupu ya Kombe la Dunia - ambayo hutoka kwenye hifadhi ya karibu $23m (£19m) zilizofunguliwa na serikali ya Senegal kulipia gharama za Kombe la Dunia - zitatofautiana kutegemea na ushiriki wa wachezaji 26 katika kampeni nzima, ikiwa ni pamoja na kufuzu.

Hata hivyo, baadhi ya wachezaji wa zamani na wanamichezo wengine wa Senegal wametilia shaka hatua hiyo.

‘’Ukishinda lazima utazawadiwa, lakini ukishindwa lazima ujifunze kutokana na hilo,’’ mshambuliaji wa zamani wa Simba ya Teranga Diomansy Kamara aliambia gazeti la Stades.

Licha ya tabia yake ya ukarimu, uamuzi wa Sall haukupokelewa vyema na wanariadha kutoka kwa michezo mingine ambao kijadi hulazimika kuchukua juhudi zaidi ili kufadhili ushiriki wao wenyewe katika mashindano.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved