logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Daddy Owen azungumzia madai ya kutoka kimapenzi na 'shabiki' wake

Katika picha yake, Eve alisema yuko tayari kuachilia mwaka wa 2023.

image
na Radio Jambo

Habari09 January 2023 - 04:04

Muhtasari


•Madai kwamba wawili hao wako kwenye mahusiano yaliibuka baada ya mashabiki kugundua kuwa walikuwa wamechapisha picha iliyopigwa katika eneo moja.

•"Katika picha hiyo, tulikuwa tu tukibarizi pamoja na watu wengine," Owen alisema.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Daddy Owen amekanusha madai kwamba anachumbiana na rafiki yake wa karibu Eve Maina.

Madai kwamba wawili hao wako kwenye mahusiano yaliibuka baada ya mashabiki kugundua kuwa walikuwa wamechapisha picha iliyopigwa katika eneo moja.

Katika picha yake, Eve alisema yuko tayari kuachilia mwaka wa 2023.

"Sipunguzi kasi kwa mtu yeyote." alisema.

Owen alisema Mungu huwapata watu hata katikati ya matatizo yoyote. Akizungumza na Word Is, Owen alisema Eve ni rafiki tu.

"Anachumbiana na sina nia ya kuchumbiana naye. Tumekuwa marafiki kwa muda mrefu," alisema.

"Katika picha hiyo, tulikuwa tu tukibarizi pamoja na watu wengine."

Mwezi Oktoba 2022, Owen alichapisha picha iliyoonyesha akiwa na Eve, huku wakiwa wamevalia mavazi yanayolingana na akimrejelea kama shabiki.

Alifanya utani kuhusu picha hiyo na kusemaEve aliweka uso wa ukali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved