logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwaka huu mpango wa kando afure tumbo, apate mimba tasa! - Pastor Ezekiel

Odero alisema kuwa kuna mipango ya kando wanaishi vizuri kuliko wake halali wa ndoa.

image
na Radio Jambo

Habari15 January 2023 - 15:21

Muhtasari


• Mchungaji Odero alisema kuwa kuna mipango ya kando wanaishi vizuri kuliko wake halali wa ndoa. 

• Alisema mwaka huu watakoma kwani laana ya Mungu itawashukia ambapo watafura tumbo bila kitu ndani.

mchungaji Ezekiel Odero

Mchungaji mwenye utata, Ezekiel Odero ametamka laana kwa wanawake michepuko ambao wanasherehekea mishahara na mapato ya wanaume walio na ndoa huku wanawake halali katika ndoa hiyo wakisaga meno.

Katika video moja ambayo ilionekana Tiktok Odero akihubiri katika kanisa lake lililopo Mavueni kaunti ya Kilifi, alisema kuwa si haki hata kidogo kwa michepuko kufurahia matunda ambayo mke halali anafaa kufurahia kwenye ndoa.

Mchungaji huyo alisema kuna michepuko ambao wanaishi maisha ya starehe kutokana na pesa na mali ya mwanaume ambaye mke wake ni mtu ayayeishi maisha ya uhayawinde mkubwa.

Kila moja aende akule mshahara wa bwanake. Wewe unajua kuna watu wanaendesha magari yaliyonunuliwa na mabwana za wengine? Watu wako na maghorofa ambayo wamejengwa na mabwana za wengine. Watu wako na mashamba! Mtu anapigwa kwa nyumba na mpango wa kando ananuniliwa nyumba,” mchungaji huyo alihubiri kwa hasira.

Alitamka laana kuwa mwaka huu mwanamke yeyote ambaye ataendelea kumchuna mume wa wenyewe atapata pigo la kufura tumbo ambalo litakuwa kama ujauzito lakini hakutakuwa na ujauzito.

“Mpango wa kando ambaye ataenda kula pesa ya mume wa watu na afure tumbo, apate mimba tasa isiyo na mtoto,” Odero alitamka laana hiyo huku akiwaamrisha waumini wake kila mmoja kugeukia jirani yake na kumtaka kukasirika ili laana hiyo inate.

Mchungaji huyo amejulikana kutokana  na mahubiri yake yenye utata ambayo yamekumbatiwa pakubwa na wananchi wengi, asilimia kubwa ikiwa ni kina mama.

Mwishoni mwa mwaka jana, Odero aiwafokea watu wazima wanaosherehekea Krismasi huku akisema kuwa sherehe hizo zinafaa kuwa za watoto na mtu mzima na akili zake hafai kusherehekea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved