logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtangazaji Gidi amuomboleza mwanafamilia wake mdogo

Pendo ambaye alikuwa na umri wa miaka 7 pekee alikata roho mwendo wa saa mbili usiku, siku ya Jumapili.

image
na Radio Jambo

Habari16 January 2023 - 04:12

Muhtasari


•Gidi alifichua kwamba mpwa wake Pendo aliaga dunia siku ya Jumapili jioni katika Hospitali ya Metropolitan.

•Gidi aliongeza kuwa familia itatoa maelezo zaidi kuhusu mipango na tarehe ya mazishi hivi karibuni

Mtangazaji mkuu wa kipindi cha Gidi na Ghost Asubuhi kwenye Radio Jambo, Joseph Ogidi almaarufu Gidi amefiwa na mpwa wake.

Gidi alifichua kwamba Baby Pendo ambaye ni binti pekee wa dada yake aliaga dunia siku ya Jumapili jioni katika Hospitali ya Metropolitan.

Pendo ambaye alikuwa na umri wa miaka 7 tu alikata roho mwendo wa saa mbili usiku, siku ya Jumapili.

"Tulikuwa na usiku mrefu lakini wacha nishukuru hospitali, jirani yangu Wakili na marafiki ambao walituunga mkono katika mchakato wa kuhamisha mwili wake hadi chumba cha kuhifadhi maiti," Gidi alitangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram siku ya Jumatatu asubuhi.

Mtangazaji huyo mahiri aliongeza kuwa familia itatoa maelezo zaidi kuhusu mipango na tarehe ya mazishi hivi karibuni.

Pia alifahamisha mtu yeyote aliye na nia ya kutoa msaada wa aina yoyote kwa maziko ya mpwa wake kuwasiliane naye.

"Roho ya Mtoto Pendo ipumzike kwa amani,” alisema.

 Sote katika Radio Jambo tunaitakia familia ya Gidi amani na nguvu na wanapomuomboleza mmoja wao. Roho ya Pendo ipumzike kwa amani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved