logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii Rayvanny ampoteza kaka yake-Baba Levo afichua

alitumia akaunti yake ya Instagram kumpa pole mwanamuziki huyo

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2023 - 12:56

Muhtasari


  • Kulingana na chapisho lililosambazwa na mtangazaji wa redio ya Wasafi, Baba Levo, kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram, mwanamuziki huyo kwa sasa anaomboleza kifo cha kaka yake
Rayvanny ajitosa siasani

Staa wa bongo kutoka Tanzania Rayvanny amempoteza kaka yake.Habari hizi zilifichuliwa na mtangazaji wa Wasafi Babalevo.

Kulingana na chapisho lililosambazwa na mtangazaji wa redio ya Wasafi, Baba Levo, kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram, mwanamuziki huyo kwa sasa anaomboleza kifo cha kaka yake.

Baba Levo ambaye pia ni mwanamuziki na rafiki wa karibu wa Rayvanny, alitumia akaunti yake ya Instagram kumpa pole mwanamuziki huyo ambaye kwa sasa yupo kwenye wakati mgumu sana.

"POLE SANA MDOGO WANGU @rayvanny KWA KUONDOKEWA NA KAKA YAKO…!MUNGU AKUPE NGUVU KWENYE KIPINDI HICHI KIGUMU🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼,"Aliandika BabaLevo.

Mashabiki walitoa pole zao kwa msanii huyo na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

mbeyadreadlocks_clinic: Pole sana rayvnny mungu akutie nguvu sana

kakole_de_santox: Duuuh 😢😢 pole ndugu yetu

amodaneissaamir: Pole rayvanny mungu akupe nguvu kwenye kipindi hichi😢

fatuma_machemba: Mm nilisema wanagombana ndugu huu uchimbii (uchuro)toka lini ndugu wakagombana hazarani😢😢pole Sana

Haya yanajiri siku chache baada ya Rayvanny na mwanamuziki mwenzake, Harmonize, kuhusika kwenye vita mtandaoni kuhusu nani ni bora kuliko mwingine.

Ugomvi wa mtandaoni iliyovuta hisia za watumiaji wengi wa mtandao na mashabiki wa pande zote mbili.

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved