logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jay Melody afichua wasanii Wakenya anaowashabikia sana

Pia alidokeza kuwa alikabiliwa na tatizo la kukataliwa na baadhi ya wasanii wakubwa

image
na Radio Jambo

Habari03 February 2023 - 08:37

Muhtasari


  • Melody aliweka wazi kwamba taaluma yake ya muziki ilingo'a nanga vizuri takriban miaka sita iliyopita baada ya kuwachia kibao 'Goroka'

Studioni katika kipindi cha ilikuaje tulikuwa naye msanii maarufu kutoka Tanzania Jay Melody ambaye amezungumzia safari yake ya usanii.

Melody aliweka wazi kwamba taaluma yake ya muziki ilingo'a nanga vizuri takriban miaka sita iliyopita baada ya kuwachia kibao 'Goroka'

Pia alidokeza kuwa alikabiliwa na tatizo la kukataliwa na baadhi ya wasanii wakubwa wakati bado akiwa msanii chipukizi.

"Kuna wasanii wakubwa unajitahidi kufanya kazi nao lakini hawaoni interest. Wakati mwingine unaweza ukaweka vesi yako kwa wimbo kisha ikatolewa kwa sababu bado hujapata kusikika. Lakini sasa siwezi kukataliwa mimi ni msanii mkubwa,"

Melody aliweka wazi kwamba kuna baadhi ya wasanii ambao ana washabikia sana nchini kenya, miongoni mwao;msanii Otile Brown,Jovial,Mejja,Msauti miongoni mwa wasanii wengine.

"Wasanii wa Kenya ambao nawashabikia sana ni,Jovial,Otile,Mejja,masauti na wengine wengi ambao nawapenda kwa ajili ya kazi ya nzuri."

Mwimbaji huyo wa kibao 'Sugar' alikiri kuwa mwanzoni alikabiliwa na changamoto kubwa ya kuwaaminisha watu kuwa anajua kuimba.

Alisema kuwa nyimbo za Kenya zinachezwa na kupendwa sana nchini Tanzania hasa jijini Dar es Salaam.

Wakati wa mahojiano hayo, mwanamuziki huyo kijana pia alifunguka kuhusu safari yake ya muziki kuanzia akiwa mwandishi wa nyimbo hadi kuimba nyimbo zake.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved